-
Kuzaa Matunda Kama Matawi na Kuwa Rafiki za YesuYesu—Njia, Kweli, na Uzima
-
-
“[Baba yangu] huliondoa kila tawi ndani yangu lisilozaa matunda, naye hulisafisha kila tawi linalozaa matunda, ili lizae matunda zaidi. . . . Kama vile tawi lisivyoweza kuzaa matunda likiwa peke yake lisipobaki katika mzabibu, vivyo hivyo hamwezi kuzaa matunda msipokaa katika muungano pamoja nami. Mimi ndiye mzabibu; nanyi ndio matawi.”—Yohana 15:2-5.
-
-
Kuzaa Matunda Kama Matawi na Kuwa Rafiki za YesuYesu—Njia, Kweli, na Uzima
-
-
Anaeleza hivi: “Yeyote anayekaa katika muungano pamoja nami, nami katika muungano pamoja naye, huyo huzaa matunda mengi; kwa maana bila mimi hamwezi kufanya lolote kamwe.” Matawi hayo—wafuasi wake waaminifu—wangezaa matunda mengi, kwa kuiga sifa za Yesu, na kuwahubiria wengine kuhusu Ufalme wa Mungu, na kufanya wanafunzi wengi. Namna gani mtu asipobaki katika muungano na Yesu na akose kuzaa matunda? Yesu anaeleza hivi: “Ikiwa yeyote hakai katika muungano pamoja nami, atatupwa.” Kwa upande mwingine, Yesu anasema: “Mkikaa katika muungano pamoja nami, na maneno yangu yakae ndani yenu, ombeni chochote mnachotaka nanyi mtapewa.”—Yohana 15:5-7.
-