Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yehova Anawapenda Wale ‘Wanaozaa Matunda kwa Uvumilivu’
    Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2018 | Mei
    • 7. (a) Ni nani wanaowakilishwa na “mkulima,” “mzabibu,” na “matawi”? (b) Tungependa kupata jibu la swali gani?

      7 Soma Yohana 15:1-5, 8. Ona kwamba Yesu aliwaambia hivi mitume wake: “Baba yangu hutukuzwa kwa jambo hili, kwamba mwendelee kuzaa matunda mengi na kujithibitisha kuwa wanafunzi wangu.” Yesu alisema kwamba Yehova “ndiye mkulima,” akasema yeye mwenyewe “ndiye mzabibu wa kweli,” na wanafunzi wake ni “matawi.”b Hivyo basi, matunda ambayo wafuasi wa Kristo wanapaswa kuzaa ni nini? Katika mfano huo, Yesu hakutaja moja kwa moja matunda hayo ni nini lakini alitaja jambo fulani muhimu linaloweza kutusaidia kujua maana ya matunda hayo.

      8. (a) Katika mfano wa Yesu, kwa nini matunda tunayopaswa kuzaa si wanafunzi tunaowasaidia kufikia hatua ya kubatizwa? (b) Ukweli ni nini kuhusu yale ambayo Yehova anataka tutimize?

      8 Yesu alisema hivi kumhusu Baba yake: “Yeye huliondoa kila tawi ndani yangu lisilozaa matunda.” Kwa maneno mengine, Yehova anatuona kuwa watumishi wake ikiwa tu tunazaa matunda. (Mt. 13:23; 21:43) Hivyo, katika mfano huo, hatuwezi kusema kwamba matunda ambayo kila Mkristo anapaswa kuzaa ni wanafunzi tunaowasaidia kufikia hatua ya kubatizwa. (Mt. 28:19) Hilo lingemaanisha kwamba Mashahidi waaminifu ambao hawajafanikiwa kumsaidia yeyote kufikia hatua ya kubatizwa kwa sababu katika eneo wanalohubiri watu hawapendezwi sana na ujumbe wetu, ni matawi yasiyozaa matunda yanayotajwa katika mfano wa Yesu. Hata hivyo, wazo hilo si sahihi hata kidogo! Kwa nini? Kwa sababu hatuwezi kuwalazimisha watu wawe wanafunzi wa Yesu. Kwa kuwa Yehova ni Mungu mwenye upendo, hawezi kamwe kuwaomba watumishi wake wafanye mambo yanayopita uwezo wao. Sikuzote Yehova hutuomba tufanye mambo tuliyo na uwezo wa kuyatimiza.—Kum. 30:11-14.

      9. (a) Tunazaa matunda tunapofanya kazi gani? (b) Tutachunguza mfano gani, na kwa nini?

      9 Hivyo basi, matunda tunayopaswa kuzaa ni nini? Ni wazi kwamba tunda linalorejelewa ni jambo ambalo kila mmoja wetu ana uwezo wa kutimiza. Ni jambo gani hilo linalowakilishwa na ‘kuzaa matunda’? Ni kazi ya kuhubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu.c (Mt. 24:14) Mfano wa Yesu kuhusu mpandaji unatusaidia kuelewa wazi jambo hilo. Acheni tuchunguze mfano huo wa pili.

  • Yehova Anawapenda Wale ‘Wanaozaa Matunda kwa Uvumilivu’
    Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2018 | Mei
    • b Ingawa katika mfano huu matawi yanawarejelea wale walio na tumaini la kuishi mbinguni, kuna mambo fulani muhimu yaliyo katika mfano huo yanayoweza kuwanufaisha watumishi wote wa Mungu.

      c Ingawa maneno ‘kuzaa matunda’ yanahusu pia kusitawisha sifa za “tunda la roho,” katika makala hii na ile itakayofuata, tutakazia kumtolea Mungu “tunda la midomo yetu,” yaani kuhubiri kuhusu Ufalme.—Gal. 5:22, 23; Ebr. 13:15.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki