-
Mambo Makuu Katika Kitabu cha YohanaMnara wa Mlinzi—2008 | Aprili 15
-
-
19:11—Je, Yesu alikuwa akizungumza kumhusu Yuda Iskariote alipokuwa akiongea na Pilato kuhusu mtu ambaye Alimtia mikononi mwake? Yesu hakuwa akizungumza kuhusu Yuda au mtu fulani hususa, bali inaonekana kwamba alimaanisha watu wote waliokuwa na hatia ya kushiriki katika dhambi ya kumuua. Hao walitia ndani Yuda, “wakuu wa makuhani na Sanhedrini nzima,” na hata “umati” ulioshawishiwa kuomba Baraba afunguliwe.—Mt. 26:59-65; 27:1, 2, 20-22.
-
-
Mambo Makuu Katika Kitabu cha YohanaMnara wa Mlinzi—2008 | Aprili 15
-
-
14:26; 16:13. Roho takatifu ya Yehova inatufundisha na kutukumbusha mambo. Pia inafunua kweli. Hivyo, inaweza kutusaidia kuongeza ujuzi, hekima, ufahamu, utambuzi, na uwezo wa kufikiri. Hivyo, tunapaswa kudumu katika sala, na kusema waziwazi katika sala kwamba tunahitaji roho hiyo.—Luka 11:5-13.
-