Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Wale Wanaoitwa ‘Miungu’”
    Amkeni!—2005 | Aprili 22
    • Hata hivyo, huenda mtu akauliza, ‘Yesu ni “Mungu Mwenye Nguvu,” katika maana gani, na je, mtume Yohana hakusema kwamba Yesu mwenyewe ni Mungu?’ Katika tafsiri ya Biblia ya Union Version, andiko la Yohana 1:1 linasema: “Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.” Watu fulani hudai kwamba “Neno,” aliyezaliwa duniani akiwa Yesu, ndiye Mungu Mweza-Yote mwenyewe. Je, ni kweli?

      Mstari huo ukifasiriwa kumaanisha kwamba Yesu ndiye Mungu Mweza-Yote mwenyewe, basi utapinga taarifa inayotangulia ya kwamba “Neno alikuwako kwa Mungu.” Mtu aliye “kwa” mwingine hawezi kuwa mtu yuleyule. Tafsiri nyingi za Biblia huonyesha tofauti iliyopo, zikitaja waziwazi kwamba Neno hakuwa Mungu Mweza-Yote. Kwa mfano, tafsiri mbalimbali za Biblia zinasema hivi: “Neno alikuwa mungu,” na “Neno alikuwa na sifa za Mungu.”a

      Mistari ya Biblia ambayo katika lugha ya Kigiriki inafanana na Yohana 1:1 hutumia neno “mungu.” Kwa mfano, umati ulisema hivi kumhusu Herode Agripa wa Kwanza: ‘Ni sauti ya mungu.’ Na wakati ambapo Paulo hakufa baada ya kuumwa na nyoka mwenye sumu, watu walisema: “Yeye ni mungu.” (Matendo 12:22; 28:3-6) Kusema kwamba Neno ni “mungu” wala si Mungu, kunapatana na sarufi ya Kigiriki na mafundisho ya Biblia.—Yohana 1:1.

      Hebu fikiria jinsi Yohana alivyomtambulisha “Neno” katika sura ya kwanza ya Injili yake. Aliandika: “Neno akawa mwili, akakaa katikati yetu, nasi tukautazama utukufu wake, utukufu kama ule ulio [si wa Mungu bali] wa mwana mzaliwa-pekee kutoka kwa baba.” Kwa hiyo, “Neno,” aliyekuwa mwili, aliishi duniani akiwa Yesu na watu walimwona. Kwa hiyo, hangeweza kuwa Mungu Mweza-Yote, ambaye Yohana anasema hivi juu yake: “Hakuna mwanadamu ambaye amemwona Mungu wakati wowote.”—Yohana 1:14, 18.

  • “Wale Wanaoitwa ‘Miungu’”
    Amkeni!—2005 | Aprili 22
    • a Ona The New Testament, ya James L. Tomanek; The Emphatic Diaglott, interlinear reading, ya Benjamin Wilson; The Bible—An American Translation, ya J.M.P. Smith na E. J. Goodspeed.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki