Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • ‘Yesu Aliwapenda Mpaka Mwisho’
    ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
    • 9 Siku ya kifo chake, Yesu alionyesha kwa njia yenye kugusa moyo sana jinsi anavyohangaikia hali ya kiroho ya wale anaowapenda. Hebu wazia jinsi ilivyokuwa. Yesu alikuwa kwenye mti wa mateso, akiwa na maumivu makali sana. Ili avute pumzi, alilazimika kujiinua kwa kujisukuma kwa miguu yake. Na haikosi kufanya hivyo kulisababisha maumivu makali sana kwa kuwa uzito wa mwili wake ulizidisha majeraha ya misumari katika miguu yake huku mgongo wake uliojeruhiwa kwa mijeledi ukisuguliwa na mti. Kwa kuwa mtu anahitaji kusawazisha pumzi anapozungumza, ingekuwa vigumu kwake kuzungumza na angepata maumivu makali. Hata hivyo, kabla tu hajafa, Yesu alitaja maneno yaliyoonyesha kwamba anampenda sana mama yake, Maria. Alipomwona Maria na mtume Yohana wakiwa wamesimama karibu, Yesu alizungumza kwa sauti inayoweza kusikika na mtu aliye karibu, na kumwambia mama yake: “Mwanamke, ona! Mwana wako!” Halafu akamwambia Yohana: “Ona! Mama yako!” (Yohana 19:26, 27) Yesu alijua kwamba mtume huyo mwaminifu angemtunza Maria kimwili na kiroho vilevile.b

      Picha katika ukurasa wa 164, 165

      Wazazi wanaojali ni wenye subira na wanashughulikia mahitaji ya watoto wao

  • ‘Yesu Aliwapenda Mpaka Mwisho’
    ‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
    • b Inaonekana kufikia wakati huo Maria alikuwa mjane, na huenda bado wale watoto wake wengine hawakuwa wanafunzi wa Yesu.—Yohana 7:5.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki