-
“Nilitumwa Kufanya Hivyo”‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
-
-
19, 20. Ni kwa njia gani Yesu alionyesha kwamba kazi ya kuhubiri inahitaji kufanywa haraka?
19 Tatu, Yesu aliona kwamba huduma yake ilipaswa kufanywa haraka. Kumbuka alipozungumza na yule mwanamke Msamaria kwenye kisima nje ya jiji la Sikari. Inaonekana kwamba mitume wa Yesu hawakuona uharaka wa kuwaeleza wengine habari njema katika pindi hiyo. Yesu aliwaambia hivi: “Je, ninyi hamsemi kwamba bado kuna miezi minne kabla ya mavuno kuja? Tazama! Ninawaambia ninyi: Inueni macho yenu myatazame mashamba, kwamba ni meupe kwa ajili ya kuvunwa.”—Yohana 4:35.
20 Mfano huo wa Yesu ulitegemea majira ya wakati huo. Inaonekana kwamba ulikuwa mwezi wa Kislevu unaolingana na Novemba/Desemba (Mwezi wa 11/Mwezi wa 12). Shayiri ingevunwa miezi minne baadaye, karibu na wakati wa Pasaka, Nisani 14. Kwa hiyo, wakulima hawakuona uharaka wa kuvuna wakati huo. Bado kulikuwa na wakati wa kutosha. Namna gani kukusanywa kwa watu? Wengi walikuwa tayari kusikia, kujifunza, kuwa wanafunzi wa Kristo na kuwa na tumaini zuri ajabu ambalo Yehova aliwaahidi. Ni kana kwamba Yesu alitazama mashamba hayo ya mfano na kuyaona kuwa meupe huku nafaka zilizoiva zikipeperushwa na upepo mwanana, kuonyesha ziko tayari kuvunwa.c Wakati wa mavuno ulikuwa umefika, nayo kazi hiyo ilipaswa kufanywa haraka! Hiyo ndiyo sababu wakati watu wa jiji fulani walipotaka Yesu aendelee kukaa kwao, alisema hivi: “Lazima nitangaze habari njema ya ufalme wa Mungu kwenye majiji mengine pia, kwa sababu nilitumwa kufanya hivyo.”—Luka 4:43.
-
-
“Nilitumwa Kufanya Hivyo”‘Njoo Uwe Mfuasi Wangu’
-
-
c Kuhusiana na mstari huo, kitabu kimoja kinasema: “Nafaka zinapoiva, rangi yake ya kijani hubadilika kuwa manjano, kuonyesha kwamba ziko tayari kuvunwa.”
-