Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Ufufuo
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Andiko la Yohana 5:28, 29 linamaanisha nini? Linasema hivi: “Wale wote waliomo ndani ya makaburi ya ukumbusho wataisikia sauti yake na kutoka, wale waliotenda mambo mema kwenye ufufuo wa uzima, wale waliokuwa na zoea la kutenda mambo maovu kwenye ufufuo wa hukumu.” Yale ambayo Yesu alisema katika andiko hilo yanapaswa kueleweka kupatana na ufunuo ambao alimpa Yohana baadaye. (Ona andiko la Ufunuo 20:12, 13, lililonukuliwa katika ukurasa wa 324.) Wale ambao zamani walifanya mambo mema na pia wale ambao zamani walitenda mambo mabaya ‘watahukumiwa kila mmoja kulingana na matendo yake.’ Matendo gani? Tukiwa na maoni kwamba watu watahukumiwa kwa msingi wa yale waliyotenda katika maisha yao ya zamani, hilo halitapatana na Waroma 6:7: “Yeye ambaye amekufa ameondolewa hatia ya dhambi yake.” Pia ni jambo lisilopatana na akili kuwafufua watu ili tu waangamizwe. Kwa hiyo, katika Yohana 5:28, 29a, Yesu alikuwa akielekeza mbele kwenye ufufuo; kisha, katika sehemu inayobaki ya mstari wa 29, alikuwa akieleza matokeo baada ya wao kufanywa kuwa wanadamu wakamilifu na kuhukumiwa.

  • Ufufuo
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Ni nani watakaotiwa ndani ya ufufuo wa kuishi duniani?

      Yoh. 5:28, 29: “Msistaajabie jambo hili, kwa sababu saa inakuja ambayo wale wote waliomo ndani ya makaburi ya ukumbusho wataisikia sauti yake [sauti ya Yesu] na kutoka.” (Neno la Kigiriki linalotafsiriwa “makaburi ya ukumbusho” si wingi wa neno taʹphos [kaburi la mtu mmoja] au haiʹdes [makaburi, kaburi la wanadamu wote waliokufa] bali ni wingi wa neno mne·meiʹon [ukumbusho, kaburi la ukumbusho]. Linakazia kuhifadhi kumbukumbu ya mtu aliyekufa. Wale watakaofufuliwa na kupewa nafasi ya kuishi milele si wale ambao kumbukumbu yao imefutwa katika Gehena kwa sababu ya dhambi zisizosamehewa bali ni watu ambao Mungu atawakumbuka.—Mt. 10:28; Marko 3:29; Ebr. 10:26; Mal. 3:16.)

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki