Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi—1988 | Februari 1
    • Bila shaka, imani katika dhabihu ya Yesu ni ya muhimu kwa wote ambao wangepata msamaha wa Mungu na uhai wa milele, uwe ni uhai mbinguni au uhai katika dunia-paradiso. Kristo alionyesha jambo hilo kwenye Yohana 6:51-54, NW: “Mimi ndimi mkate hai ambao ulikuja chini kutoka mbinguni; ikiwa ye yote anakula baadhi ya mkate huu ataishi milele; . . . mkate ambao mimi nitatoa ni mnofu wangu kwa niaba ya uhai wa ulimwengu [wa aina ya wanadamu wenye kukomboleka] . . . Yeye ambaye anajilisha mnofu wangu mimi na kunywa damu yangu mimi ana uhai wa milele.”

      Hata hivyo, inastahili kuangaliwa kwamba Yesu alisema maneno hayo kwa wengine zaidi ya wanafunzi wake tu. Siku moja baada ya yeye kuwa amelisha maelfu kimuujiza, lile kutano la watu lilikuja kwa Yesu katika eneo la Kapernaumu. Kutano hilo la watu lilimhusisha yeye katika maongezi ambayo yalitia ndani maneno yake kwenye Yohana 6:51-54. Kwa hiyo Yesu hakuwa akisema hasa kwa wanafunzi wake wakati yeye aliposema kwamba yeye alikuwa ndiye ule ‘mkate ambao ulikuja chini kutoka mbinguni’ ulio wa mfano, ambao unaweza kuandaa matazamio ya uhai yenye kudumu zaidi ya ile mana ambayo ilikuwa imeliwa katika lile jangwa.​—Yohana 6:24-34.

      Katika kufikiria tukio hilo la kale katika iile jangwa, kumbuka ni nani ambao waiikuwa wametoka Misri kuingia katika lile jangwa. Walikuwa ni ‘wale wana wa Israeli wenye hesabu ya wanaume makakawana mia sita elfu wenye kutembea kwa miguu, bila kutia ndani wadogo-wadogo, na andamano-mchanganyiko lililo kubwa sana.’ (Kutoka 12:37, 38; 16:13-18, NW) Hilo “andamano-mchanganyiko” lilitia ndani Wamisri ambao walikuwa wameolewa na Waisraeli na Wamisri wengine ambao walikuwa wametupa kura yao pamoja na Waisraeli. Wote Waisraeli na lile “andamano-mchanganyiko” walihitaji mana ili kubaki hai. Ingawa hivyo, je! hilo “andamano-mchanganyiko,” lilikuwa na matazamio yale yale kama Waisraeli? Sivyo, hawakuwa nayo. Hata ingawa wao wangeweza kuabudu miongoni mwa Waisraeli na wangeweza kutumainia kuingia ile Nchi ya Ahadi, wao hawangeweza kamwe kuwa wafalme au makuhani chini ya lile agano la Sheria. Kwa hiyo kula ile mana halisi katika lile jangwa hakukumpa kila mmoja matazamio yale yale mamoja.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi—1988 | Februari 1
    • Bila shaka, Wakristo wote wa kweli leo ambao wanatazama mbele kuishi milele duniani chini ya utawala wa Ufalme wanajua kwamba jambo hilo linawezekana kwa kujizoeza imani katika dhabihu ya Yesu. Kama vile Yesu alivyoambia lile kutano la watu, yeye ndiye “mkate hai ambao ulikuja chini kutoka mbinguni.” (Yohana 6:51, NW) Hata hivyo, hilo halimaanishi kwamba wale waiio na lile tumaini la kidunia wanapaswa kushiriki sehemu ya ile mifano halisi ya Ukumbusho, kwa maana wao hawamo katika “lile agano jipya,” wala wao hawamo katika lile agano pamoja na Yesu kuwa ‘katika ufalme wake, wakiketi juu ya viti vya ufalme.’

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki