Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mtumikie Yehova Bila Kukengeuka
    Mnara wa Mlinzi—2015 | Oktoba 15
    • 1, 2. Kwa nini Yesu alimpenda Martha? Lakini tunajuaje kwamba Martha hakuwa mkamilifu?

      UNAFIKIRI Martha alikuwa mtu wa aina gani? Yeye ndiye mwanamke pekee anayetajwa kwa jina kwamba alipendwa na Yesu. Bila shaka, Yesu aliwapenda wanawake wengine waliomtumikia Mungu kama vile mama yake mpendwa na Maria dada ya Martha. (Yoh. 11:5; 19:25-27) Hata hivyo, kwa nini Yesu alimpenda Martha?

  • Mtumikie Yehova Bila Kukengeuka
    Mnara wa Mlinzi—2015 | Oktoba 15
    • 4 Hata hivyo, Martha alikuwa na shughuli nyingi akitayarisha mlo na kufanya kazi nyingine ili tukio hilo liwe la pekee. Lakini mambo hayo yalimsababishia mahangaiko yasiyo ya lazima, na kufanya amkasirikie Maria. Yesu alitambua kwamba Martha anahangaikia mambo mengi, hivyo akamwambia hivi kwa upole: “Martha, Martha, wewe unahangaika na kusumbuka juu ya mambo mengi.” Kisha akasema kwamba hata mlo mmoja tu ungetosha. Halafu Yesu akamgeukia Maria na kumwondolea wasiwasi kwa kusema hivi: “Maria alichagua fungu jema, nalo halitaondolewa kwake.” Baada ya muda mfupi, Maria angesahau chakula walichokula wakati huo, lakini hangesahau kamwe pongezi na mambo aliyofundishwa na Yesu. Zaidi ya miaka 60 baadaye, mtume Yohana aliandika hivi: “Yesu alimpenda Martha na dada yake.” (Yoh. 11:5) Maneno hayo yanaonyesha kwamba Martha alikubali kurekebishwa na Yesu na akajitahidi kumtumikia Yehova kwa uaminifu maishani mwake.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki