-
Kuhani Mkuu Aliyemhukumu YesuMnara wa Mlinzi—2006 | Januari 15
-
-
Uovu wa Kayafa ulifunuliwa wakati alipowaambia watawala wenzake hivi: “Hamwoni kwamba ni kwa faida yenu mtu mmoja afe kwa ajili ya watu kuliko taifa lote liangamizwe.” Simulizi hilo linaendelea kusema hivi: “Ingawa hivyo, hilo hakulisema kwa kujitungia mwenyewe; lakini kwa sababu alikuwa kuhani mkuu mwaka huo, alitoa unabii kwamba Yesu alikusudiwa kufa kwa ajili ya taifa, na si kwa ajili ya taifa hilo tu, bali ili watoto wa Mungu waliotawanyika huku na huku yeye apate pia kuwakusanya pamoja kuwa mmoja. Kwa hiyo tangu siku hiyo na kuendelea wakakata shauri kumuua [Yesu].”—Yohana 11:49-53.
Kayafa hakujua maana kamili ya maneno yake. Kwa kuwa alikuwa kuhani mkuu, alitoa unabii.b Si Wayahudi tu ambao wangefaidika na kifo cha Yesu. Dhabihu yake ya fidia ingewawezesha wanadamu wote kukombolewa kutoka katika utekwa wa dhambi na kifo.
-
-
Kuhani Mkuu Aliyemhukumu YesuMnara wa Mlinzi—2006 | Januari 15
-
-
b Zamani, Yehova alimtumia Balaamu mwovu kutoa unabii mbalimbali wa kweli kuhusu Waisraeli.—Hesabu 23:1–24:24.
-