Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Wamtafute Mungu, . . . na kwa Kweli Wampate”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
    • 17, 18. Kwa nini wanadamu wanapaswa kumkaribia Mungu, nasi tunaweza kujifunza nini kutokana na jinsi Paulo alivyozungumza na wasikilizaji wake?

      17 Wanadamu wanapaswa kumkaribia Mungu. Paulo alisema kwamba, kwa sababu ya Mungu “tuko hai, tunatembea, na tunaishi.” Wasomi fulani husema kwamba Paulo alikuwa akirejelea maneno ya Epimenide, mshairi Mgiriki wa karne ya sita K.W.K. “aliyeheshimiwa sana katika utamaduni wa dini ya Waathene.” Paulo alitaja sababu nyingine inayopaswa kuwafanya wanadamu wahisi wako karibu na Mungu, aliposema: “Baadhi ya washairi wenu wamesema, ‘Kwa maana sisi pia ni watoto wake.’” (Mdo. 17:28) Wanadamu wanapaswa kujiona kuwa na uhusiano wa karibu sana na Mungu, kwa kuwa Yeye ndiye Baba ya mwanadamu wa kwanza ambaye wanadamu wote walitoka kwake. Ili kuwavutia wasikilizaji wake, Paulo alitumia busara kwa kunukuu moja kwa moja vitabu vya Kigiriki ambavyo bila shaka watu waliomsikiliza waliviheshimu sana.e Kama Paulo, nyakati nyingine tunaweza kunukuu vitabu vya historia, ensaiklopedia, au vitabu vingine vya marejeo vinavyoheshimika. Kwa mfano, nukuu inayofaa kutoka katika chanzo kinachotegemeka, inaweza kumsaidia mtu ambaye si Shahidi kujua chanzo cha mazoea au maadhimisho fulani ya dini za uwongo.

  • “Wamtafute Mungu, . . . na kwa Kweli Wampate”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
    • e Paulo alinukuu shairi linaloitwa Phaenomena, la Arato, mshairi Mstoa. Maneno kama hayo yanapatikana katika vitabu vingine vya Kigiriki kutia ndani wimbo unaoitwa Hymn to Zeus, uliotungwa na Kleanthe, mwandikaji Mstoa.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki