Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Endelea Kusema na Usinyamaze”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
    • 8, 9. Paulo alifanya nini alipopingwa na Wayahudi aliowahubiria, naye alienda kuhubiri wapi?

      8 Paulo aliiona kazi ya kimwili kuwa njia ya kumtegemeza katika huduma yake. Hilo lilionekana wazi Sila na Timotheo walipowasili kutoka Makedonia wakiwa na zawadi nyingi. (2 Kor. 11:9) Mara moja, Paulo “akaanza kushughulika sana na lile neno [“alianza kutumia wakati wake wote kwa ajili ya kuhubiri,” Biblia Habari Njema].” (Mdo. 18:5) Hata hivyo, Wayahudi aliowahubiria walimpinga. Alijiondolea lawama kwa sababu walikataa ujumbe unaookoa uhai kumhusu Kristo. Paulo alikung’uta mavazi yake na kuwaambia Wayahudi hao waliompinga: “Damu yenu na iwe juu ya vichwa vyenu wenyewe. Mimi ni safi. Kuanzia sasa nitaenda kwa watu wa mataifa.”​—Mdo. 18:6; Eze. 3:18, 19.

  • “Endelea Kusema na Usinyamaze”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
    • 10. Ni nini kinachoonyesha kwamba Paulo hakuazimia kuwahubiria tu watu wa mataifa?

      10 Paulo aliposema angeenda kwa watu wa mataifa, je alimaanisha hangewahubiria kabisa Wayahudi na Wayahudi wageuzwa imani, kutia ndani wale waliokubali ujumbe wake? Hapana. Kwa mfano, “Krispo, ofisa msimamizi wa sinagogi akamwamini Bwana, yeye pamoja na watu wote wa nyumba yake.” Inaonekana kwamba wengi kati ya wale waliokuwa wakienda katika sinagogi walijiunga na Krispo, kwa sababu Biblia inasema: “Wakorintho wengi waliosikia wakaanza kuamini na kubatizwa.” (Mdo. 18:8) Basi, kutaniko jipya la Kikristo lililoanzishwa jijini Korintho likaanza kukutanika katika nyumba ya Titio Yusto. Ikiwa masimulizi ya kitabu cha Matendo yanafuata mtindo wa Luka—yaani, yanafuatana kulingana na wakati yalipotukia—basi hilo linamaanisha kwamba Wayahudi hao au Wayahudi wageuzwa imani walikuwa Wakristo baada ya Paulo kukung’uta mavazi yake. Ikiwa ndivyo, basi ni wazi kwamba Paulo alikuwa tayari kubadilika kulingana na hali.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki