-
Korintho—Jiji la Bahari MbiliAmkeni!—1991 | Novemba 8
-
-
Lile Baraza—mahali pa kuvutia kama nini! Limefanyizwa na michongo miwili yenye umbo wa mstatili katika mhimili ya mashariki-magharibi. Katikati ya mchongo wa juu, ukizungukwa na maduka pande zote mbili, kuna jukwaa lililoinuka linaloitwa bema, lililotumiwa na wasemaji katika vipindi rasmi. Kiongozi wetu alitukumbusha kwamba wakati tabibu Luka alipoandika juu ya siku ya Paulo mahakamani mbele ya Liwali Galio, neno la kigiriki lililotumiwa kwa “kiti cha hukumu” lilikuwa ni bema. (Matendo 18:12) Hivyo, matukio ya Matendo 18:12-17 huenda yalitukia mahali papo hapo! Tulikuwa tumesimama mahali ambapo yaelekea Paulo angesimama, tayari kujitetea huku amezungukwa na Wayahudi wanaomshtaki. Lakini la! Galio haisikizi kesi hiyo. Badala yake aachilia Paulo na kuruhusu umati wenye jeuri kumcharaza Sosthene.
-
-
Korintho—Jiji la Bahari MbiliAmkeni!—1991 | Novemba 8
-
-
[Picha katika ukurasa wa 17]
Juu: Duka lililojengwa upya katika lile Baraza
Katikati: Ile “bema”
-