-
Yohana Mbatizaji Atayarisha NjiaYesu—Njia, Kweli, na Uzima
-
-
Ujumbe wa Yohana unawasisimua watu wanaokuja kumsikiliza. Wengi wanatambua kwamba wanahitaji kutubu, yaani kubadili mtazamo na mwenendo wao, wakiacha maisha yao ya zamani ambayo hayafai. Wale ambao wamemjia wanatoka “Yerusalemu na Yudea yote na maeneo yote yaliyo karibu na Yordani.” (Mathayo 3:5) Wengi kati ya wale ambao wamekuja kwa Yohana, wanatubu. Anawabatiza kwa kuwazamisha katika maji ya mto Yordani. Kwa nini?
Anawabatiza watu ili waonyeshe, au kukubali kwamba wametubu kutoka moyoni dhambi walizotenda dhidi ya agano la Sheria ya Mungu. (Matendo 19:4) Hata hivyo si wote wanaostahili. Baadhi ya viongozi wa kidini, Mafarisayo na Masadukayo, wanapomjia Yohana, anawaita “uzao wa nyoka.” Anawaambia: “Zaeni matunda yanayoonyesha toba. Msithubutu kujiambia, ‘Abrahamu ndiye baba yetu.’ Kwa maana ninawaambia, Mungu anaweza kumwinulia Abrahamu watoto kutoka kwenye mawe haya. Tayari shoka limewekwa kwenye mzizi wa miti. Basi, kila mti usiozaa matunda mazuri utakatwa na kutupwa motoni.”—Mathayo 3:7-10.
-
-
Yohana Mbatizaji Atayarisha NjiaYesu—Njia, Kweli, na Uzima
-
-
Kwa hiyo, ujumbe wa Yohana, “Tubuni, kwa maana Ufalme wa mbinguni umekaribia,” ni muhimu sana. (Mathayo 3:2) Ni tangazo la hadharani kwamba huduma ya Yesu Kristo, Mfalme anayekuja ambaye amechaguliwa na Yehova, iko karibu kuanza.
-