Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Neno la Yehova ‘Lilikua na Kusitawi’ Licha ya Upinzani
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
    • 15. Tunawezaje kuwaiga Waefeso kuhusiana na mazoea ya kuwasiliana na roho, au vitu vinavyohusiana na mazoea hayo?

      15 Ilipojulikana wazi kwamba wana wa Skewa hawana nguvu, watu wengi waliamua kuwa Wakristo na kuacha mazoea ya kuwasiliana na roho. Waefeso wengi waliamini mambo ya uchawi. Watu walifanya mambo ya uchawi na walikuwa na vitu na vitabu vingi vilivyohusiana na mambo hayo. Hivyo, Waefeso wengi walichochewa kutoa vitabu vyao vya uchawi na kuviteketeza hadharani. Kulingana na viwango vya leo, vitabu hivyo vilikuwa na thamani ya pesa nyingi sana.d Luka anasema: “Hivyo kwa njia yenye nguvu, neno la Yehova likazidi kukua na kusitawi.” (Mdo. 19:17-20) Ulikuwa ushindi mkubwa wa ile kweli dhidi ya uwongo na roho waovu! Watu hao waaminifu walituwekea mfano mzuri tunaoweza kuiga leo. Sisi pia tunaishi katika ulimwengu ambao watu wengi wana mazoea ya kuwasiliana na roho. Tukigundua kwamba tuna kitu fulani kinachohusiana na mazoea hayo, tunapaswa kufanya kama walivyofanya Waefeso—kukiharibu kabisa! Na tuepuke kabisa mazoea hayo yenye kuchukiza, hata ikiwa ni vigumu kufanya hivyo.

  • Neno la Yehova ‘Lilikua na Kusitawi’ Licha ya Upinzani
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
    • d Kulingana na Luka, vitabu hivyo viligharimu vipande 50,000 vya fedha. Ikiwa alikuwa akizungumzia dinari, basi mfanyakazi wa nyakati hizo angehitaji kufanya kazi kila siku kwa siku 50,000—miaka 137 hivi ili kupata pesa hizo.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki