-
Yesu Ana Sifa Gani?Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
6. Yesu ni mkarimu
Yesu alikuwa mkarimu ingawa hakuwa na vitu vingi vya kimwili, na alitutia moyo tuwe wakarimu. Soma Matendo 20:35, kisha mzungumzie swali hili:
Kulingana na maneno hayo ya Yesu, tunawezaje kuwa na furaha?
Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali linalofuata.
Tunaweza kutoa katika njia zipi, hata ikiwa hatuna vitu vingi vya kimwili?
-
-
Maoni ya Biblia Kuhusu Pesa na KaziFurahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
3. Tunawezaje kutumia pesa zetu kwa ukarimu?
Yehova ni Mungu mkarimu na tunamwiga tunapokuwa “wakarimu, tayari kushiriki vitu na wengine.” (1 Timotheo 6:18) Tunaweza kutumia pesa zetu kwa ukarimu kwa kutoa michango katika kutaniko na kuwasaidia watu wengine wanaohitaji msaada, hasa waabudu wenzetu. Yehova anapendezwa hasa na nia yetu ya kutoa, bali si kiasi tunachotoa. Tunapotoa kwa ukarimu kutoka moyoni, tunakuwa na furaha na tunamfurahisha Yehova.—Soma Matendo 20:35.
-