-
“Nisikilizeni Ninapojitetea”“Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
-
-
11. Wazee walimwagiza Paulo afanye nini, na huenda ni nini kilichohusika? (Ona pia maelezo ya chini.)
11 Ijapokuwa uvumi uliokuwa umeenea haukuwa wa kweli, bado uliwasumbua waamini Wayahudi. Ndiyo sababu wazee walimwagiza Paulo: “Tuna wanaume wanne waliojiwekea nadhiri. Nenda pamoja na watu hawa ukajitakase kisherehe pamoja nao na kuwagharimia, ili wanyolewe vichwa vyao. Ndipo kila mtu atajua kwamba uvumi walioambiwa kukuhusu si wa kweli, bali unatembea kwa utaratibu, na pia unashika Sheria.”c—Mdo. 21:23, 24.
12. Paulo alionyeshaje kwamba alikuwa tayari kubadilika kulingana na hali na kufuata maagizo ya wazee wa Yerusalemu?
12 Paulo angeweza kushikilia msimamo wake na kudai kwamba tatizo si uvumi ulioenea kumhusu, bali ni maoni ya waamini hao Wayahudi kuhusu Sheria ya Musa. Badala ya kufanya hivyo, alikuwa tayari kubadilika kulingana na hali maadamu kufanya hivyo hakungevunja viwango vya Mungu. Mapema alikuwa ameandika hivi: “Kwa wale walio chini ya sheria nilikuwa kama aliye chini ya sheria, ingawa mimi mwenyewe siko chini ya sheria, ili niwapate wale walio chini ya sheria.” (1 Kor. 9:20) Katika kisa hiki, Paulo aliamua kufuata maagizo ya wazee wa Yerusalemu na kuwa “kama aliye chini ya sheria.” Kwa kufanya hivyo, alituwekea kielelezo kizuri cha kufuata maagizo ya wazee badala ya kuamua kufanya mambo kwa njia yetu.—Ebr. 13:17.
Ikiwa hakuna kanuni za Kimaandiko zilizohusika, Paulo alikuwa tayari kubadilika kulingana na hali. Je, wewe hufanya hivyo?
-
-
“Nisikilizeni Ninapojitetea”“Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
-
-
c Wasomi fulani wanadokeza kwamba watu hao walikuwa wameweka Nadhiri. (Hes. 6:1-21) Ni kweli kwamba Sheria ya Musa, iliyotumika kuweka nadhiri hizo, haikuwa ikitumika tena. Hata hivyo, huenda Paulo aliona kwamba hakuna ubaya kwa watu hao kutimiza nadhiri waliyoweka kwa Yehova. Kwa hiyo, haingekuwa vibaya kulipa gharama zao na kuandamana nao. Hatujui ni nadhiri ya aina gani iliyowekwa, hata hivyo, haielekei kwamba Paulo angeshiriki kutoa dhabihu ya mnyama (kama Wanadhiri walivyofanya), akiamini kwamba ingesafisha dhambi za mtu. Dhabihu kamilifu ya Kristo ilikuwa imeondolea mbali uwezo wa dhabihu hizo kusafisha dhambi. Vyovyote vile, tuna hakika kwamba Paulo hangekubali kufanya chochote ambacho kingechafua dhamiri yake.
-