-
“Jipe Moyo!”“Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
-
-
10. Paulo alishtakiwa mambo gani mazito?
10 Akiwa Kaisaria, Paulo ‘aliwekwa chini ya ulinzi katika jumba la kifalme la Herode’ akingojea waliomshtaki wafike kutoka Yerusalemu. (Mdo. 23:35) Siku tano baadaye, wakafika—Kuhani Mkuu Anania, wakili anayeitwa Tertulo, na kikundi cha wazee. Tertulo alianza kwa kumsifu Feliksi kwa mambo aliyokuwa akiwafanyia Wayahudi, huenda ili apate kibali chake.b Kisha, akianza mashtaka yake, Tertulo alisema kwamba Paulo ni “msumbufu, akichochea uasi miongoni mwa Wayahudi wote katika dunia yote inayokaliwa, naye ni kiongozi wa madhehebu ya Wanazareti. Pia alijaribu kulichafua hekalu, basi tukamkamata.” Wale Wayahudi wengine “wakajiunga katika shambulio hilo, wakisisitiza kwamba mambo hayo ni ya kweli.” (Mdo. 24:5, 6, 9) Kuchochea uasi, kuongoza madhehebu hatari, na kulichafua hekalu—hayo yalikuwa mashtaka mazito ambayo yangeweza kufanya mtu ahukumiwe kifo.
-
-
“Jipe Moyo!”“Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
-
-
b Tertulo alimshukuru Feliksi kwa “amani nyingi” aliyoileta katika taifa hilo. Hata hivyo, ukweli ni kwamba amani iliyokuwa Yudea Feliksi akiwa gavana, ilikuwa ndogo ukilinganisha na amani nyingi iliyokuwako wakati wa wale magavana wengine waliotangulia mpaka uasi dhidi ya Roma ulipotokea. Pia, hakusema kweli alipotaja kwamba Wayahudi walitoa “shukrani nyingi sana” kwa marekebisho ambayo Feliksi alikuwa amefanya. Ukweli ni kwamba Wayahudi wengi walimchukia Feliksi kwa sababu ya kuwakandamiza na kuwatendea kikatili walipoasi.—Mdo. 24:2, 3.
-