-
“Mimi Nakata Rufani kwa Kaisari!”Mnara wa Mlinzi—2001 | Desemba 15
-
-
Kuhani wa Cheo cha Juu Anania, wanaume wazee Wayahudi, na Tertulo walimshtaki Paulo rasmi mbele ya Feliksi kuwa ‘msumbufu na mwenye kufanya uchochezi wa uasi miongoni mwa Wayahudi.’ Walidai kwamba alikuwa kiongozi mkuu wa “farakano la Wanazareti” na kwamba alijaribu kulichafua hekalu.—Matendo 24:1-6.
Watu waliomshambulia Paulo hapo awali walidhani kwamba Paulo alimwingiza Trofimo mtu asiye Myahudi, kwenye ua uliotengwa kwa ajili ya Wayahudi peke yao.a (Matendo 21:28, 29) Kwa kweli, Trofimo alijipeleka mwenyewe kwenye ua bila ruhusa. Lakini iwapo Wayahudi waliona kosa la Paulo kuwa ni kumsaidia mtu aingie kwenye ua bila ruhusa, basi kosa hilo lingefanya mtu ahukumiwe kifo. Na yaonekana Roma ilikubali hukumu ya kifo kwa kosa hilo. Kwa hiyo, iwapo Paulo angekamatwa na polisi Wayahudi wa hekalu badala ya kukamatwa na Lisiasi, Sanhedrini ingemshtaki na kumhukumu bila tatizo lolote.
-
-
“Mimi Nakata Rufani kwa Kaisari!”Mnara wa Mlinzi—2001 | Desemba 15
-
-
a Ukuta wa mawe uliojengwa vizuri, wenye urefu upatao sentimeta 24 ulitenganisha ua wa ndani na ua wa wasio Wayahudi. Maonyo yaliandikwa kwenye ukuta huo, baadhi yake kwa Kigiriki na mengine kwa Kilatini: “Mgeni yeyote haruhusiwi kuvuka ukuta au kuingia ndani ya ua unaozunguka patakatifu. Yeyote atakayekamatwa akifanya hivyo atauawa.”
-