-
“Hakuna Hata Mmoja Wenu Atakayepotea”“Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
-
-
“Wote Wakafika Salama Kwenye Nchi Kavu” (Mdo. 27:27-44)
“Akamshukuru Mungu mbele yao wote.”—Matendo 27:35
16, 17. (a) Paulo alitumia nafasi gani kutoa sala, na matokeo yalikuwa nini? (b) Mambo aliyotabiri Paulo yalitimiaje?
16 Baada ya majuma mawili yenye kutia hofu, na baada ya meli kusukumwa na upepo kilomita 870 hivi, mabaharia hao walianza kuona ishara za mabadiliko, huenda hata walianza kusikia mawimbi yakigonga nchi kavu. Walishusha nanga kutoka kwenye tezi ili wasichukuliwe na mawimbi nao wakaanza kuielekeza meli nchi kavu endapo wangeweza kuifikisha pwani. Kisha, wakajaribu kuondoka melini lakini wakazuiwa na askari. Paulo akamwambia ofisa wa jeshi pamoja na askari hao: “Watu hawa wasipobaki katika meli, ninyi hamwezi kuokoka.” Sasa, meli ikiwa imara kiasi, Paulo aliwahimiza wale chakula, akiwahakikishia tena kwamba wataokoka. Kisha Paulo “akamshukuru Mungu mbele yao wote.” (Mdo. 27:31, 35) Kwa kutoa sala hiyo ya shukrani, Paulo aliwawekea mfano mzuri Luka, Aristarko, na Wakristo wa leo. Je, sala unazotoa mbele za wengine ni zenye kutia moyo na kuwafariji wengine?
-