Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Aliwatumia Wachache Kuwalisha Wengi
    Mnara wa Mlinzi—2013 | Julai 15
    • 8. Waamini wapya walionyeshaje katika siku ya Pentekoste kwamba walitambua waziwazi njia ambayo Kristo alikuwa akitumia?

      8 Kuanzia Pentekoste ya 33 W.K., Kristo aliyefufuliwa aliwatumia mitume wake kuwalisha wanafunzi wake wengine watiwa-mafuta. (Soma Matendo 2:41, 42.) Njia hiyo ilitambuliwa waziwazi na Wayahudi na watu waliogeuzwa imani ambao walikuja kuwa Wakristo watiwa-mafuta kwa roho siku hiyo. Bila kusitasita, ‘waliendelea kujitoa wenyewe kwa fundisho la mitume.’ Msomi mmoja anasema kwamba kitenzi cha Kigiriki kinachotafsiriwa ‘waliendelea kujitoa wenyewe’ kinaweza kumaanisha kuwa na “ushikamanifu imara katika kufuata mwendo fulani.” Waamini hao wapya walikuwa na njaa kubwa ya chakula cha kiroho, nao walijua vizuri mahali ambapo wangekipata. Wakiwa na ushikamanifu usioyumbayumba, waliwategemea mitume kufafanua maneno na matendo ya Yesu na kutoa uelewaji mpya wa maandiko kumhusu.c—Mdo. 2:22-36.

  • Aliwatumia Wachache Kuwalisha Wengi
    Mnara wa Mlinzi—2013 | Julai 15
    • c Fungu la 8: Uhakika wa kwamba waamini wapya ‘waliendelea kujitoa wenyewe kwa fundisho la mitume’ unadokeza kwamba mitume walikuwa wakifundisha kwa ukawaida. Baadhi ya mafundisho ya mitume yaliandikwa, na yamedumu katika vitabu vilivyoongozwa na roho takatifu ambavyo sasa ni sehemu ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki