Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Jinsi Habari Njema Inavyohubiriwa
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • 6. Tunatii amri ya Mungu ya kuhubiri

      Katika karne ya kwanza, wapinzani walijaribu kuwazuia wanafunzi wa Yesu ili wasihubiri. Wakristo wa mapema walitetea haki yao ya kuhubiri kwa “kuithibitisha kisheria habari njema.” (Wafilipi 1:7) Mashahidi wa Yehova wanafanya vivyo hivyo leo.a

      Onyesha VIDEO.

      VIDEO: Kuitetea Kisheria Habari Njema (2:28)

      Soma Matendo 5:27-42, kisha mzungumzie swali hili:

      • Kwa nini hatutaacha kuhubiri?​—Ona mstari wa 29, 38, na 39.

  • Inamaanisha Nini Kutounga Mkono Upande Wowote
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • Inamaanisha Nini Kutounga Mkono Upande Wowote?

      Yesu aliwafundisha wafuasi wake kwamba hawapaswi kuwa “sehemu ya ulimwengu.” (Yohana 15:19) Hilo linahusisha kutounga mkono upande wowote katika vita au siasa za ulimwengu. Ukweli ni kwamba si rahisi sikuzote kutounga mkono upande wowote. Huenda watu wakatudhihaki kwa sababu ya msimamo wetu. Tunawezaje kuepuka kuunga mkono upande wowote na kuendelea kuwa washikamanifu kwa Yehova Mungu?

      1. Wakristo wa kweli wana maoni gani kuhusu serikali za wanadamu?

      Wakristo wanaheshimu serikali. Tunatii maneno haya ya Yesu: “Mlipeni Kaisari vitu vya Kaisari.” Hilo linamaanisha tunatii sheria za nchi, kama vile kulipa kodi. (Marko 12:17) Biblia inafundisha kwamba serikali za wanadamu zinatawala kwa sababu Yehova ameruhusu ziwepo. (Waroma 13:1) Basi, tunaelewa kwamba serikali za wanadamu zina mamlaka ya kadiri au yenye mipaka. Tunaamini kwamba Mungu atatumia Ufalme wake wa mbinguni kuondoa matatizo ya wanadamu.

      2. Tunawezaje kuonyesha kwamba hatuungi mkono upande wowote?

      Kama Yesu, sisi pia hatujihusishi na siasa. Watu walipoona muujiza mmoja wa Yesu, walitaka kumfanya awe Mfalme wao duniani, lakini alikataa. (Yohana 6:15) Kwa nini alikataa? Kwa sababu baadaye alisema hivi: “Ufalme wangu si sehemu ya ulimwengu huu.” (Yohana 18:36) Tukiwa wanafunzi wa Yesu, tunaonyesha kwa njia mbalimbali kwamba hatuungi mkono upande wowote. Kwa mfano, hatushiriki katika vita. (Soma Mika 4:3.) Tunaheshimu nembo za taifa kama vile bendera, lakini hatuziabudu. (1 Yohana 5:21) Na hatuungi mkono wala kupinga mgombeaji au chama chochote cha kisiasa. Kwa kufanya hivyo, tunaonyesha kwamba sisi ni washikamanifu kabisa kwa serikali ya Mungu, yaani, Ufalme wake.

      CHIMBA ZAIDI

      Chunguza hali ambazo zinaweza kufanya iwe vigumu kutounga mkono upande wowote na jinsi unavyoweza kufanya maamuzi yanayomfurahisha Yehova.

      Mwanamume ambaye haungi mkono upande wowote. Hasikilizi wagombeaji wa kisiasa wanaopingana wakizungumza na umati wa watu.

      3. Wakristo wa kweli hawaungi mkono upande wowote

      Yesu na wafuasi wake walituwekea mfano. Soma Waroma 13:1, 5-7 na 1 Petro 2:13, 14. Kisha, onyesha VIDEO na mzungumzie maswali yanayofuata.

      VIDEO: Wakristo wa Kweli Hawaungi Mkono Upande Wowote​—Sehemu ya 1 (4:28)

      • Kwa nini tunapaswa kuheshimu serikali za wanadamu?

      • Tunaweza kuonyeshaje kwamba tunajitiisha chini ya serikali hizo?

      Wakati wa vita, huenda mataifa fulani yakadai kwamba hayaungi mkono upande wowote, lakini yanasaidia pande zote zinazozozana. Kutounga mkono upande wowote kunamaanisha nini hasa? Soma Yohana 17:16. Kisha, onyesha VIDEO na mzungumzie swali linalofuata.

      VIDEO: Wakristo wa Kweli Hawaungi Mkono Upande Wowote​—Sehemu ya 2 (3:09)

      • Inamaanisha nini kutounga mkono upande wowote?

      Tunapaswa kufanya nini ikiwa serikali za wanadamu zinatuamuru tufanye jambo linalopingana na sheria ya Mungu? Soma Matendo 5:28, 29. Kisha, onyesha VIDEO na mzungumzie maswali yanayofuata.

      VIDEO: Wakristo wa Kweli Hawaungi Mkono Upande Wowote​—Sehemu ya 3 (1:18)

      • Sheria za wanadamu zinapopingana na sheria za Mungu, tunapaswa kutii sheria za nani?

      • Unafikiri ni katika hali gani Wakristo hawapaswi kutii serikali za wanadamu?

      4. Onyesha kwamba huungi mkono upande wowote kupitia mawazo na matendo yako

      Soma 1 Yohana 5:21. Kisha, onyesha VIDEO na mzungumzie maswali yanayofuata.

      VIDEO: Wakristo wa Kweli Wanahitaji Ujasiri​—Ili Wasiunge Mkono Upande Wowote (2:50)

      • Katika video hiyo, kwa nini Ayenge alikataa kujiunga na chama cha kisiasa au kushiriki katika sherehe za kitaifa, kama vile kupiga saluti mbele ya bendera?

      • Je, unafikiri alifanya uamuzi wa hekima?

      Msimamo wetu wa kutounga mkono upande wowote unaweza kujaribiwa katika hali gani nyingine? Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali yanayofuata.

      VIDEO: Masomo Kutoka kwa Mnara wa Mlinzi​—Usiunge Mkono Upande Wowote Katika Ulimwengu Huu Uliogawanyika (5:16)

      • Tunawezaje kuonyesha kwamba hatuungi mkono upande wowote kunapokuwa na mashindano ya michezo kati ya mataifa mbalimbali?

      • Tunawezaje kuendelea kutounga mkono upande wowote, iwe maamuzi ya wanasiasa yatatunufaisha au kutuletea madhara?

      • Msimamo wetu wa kutounga mkono upande wowote unawezaje kuathiriwa na mambo tunayosikia katika vyombo vya habari au watu tunaoshirikiana nao?

      Picha: 1. Kikundi cha watu wenye hasira walio na mabango wakiandamana. 2. Mwanamume akishangilia akiwa ameshika bendera wakati wa mashindano ya michezo. 3. Mwanafunzi anaimba wimbo wa taifa. 4. Mwanajeshi akiwa amebeba bunduki. 5. Wagombeaji wawili wa kisiasa wakifanya mjadala. 6. Mwanamke anaweka kura katika sanduku wakati wa kupiga kura.

      Ni katika hali gani ambazo Mkristo anapaswa kudumisha msimamo wa kutounga mkono upande wowote kupitia mawazo na matendo yake?

      HUENDA MTU AKAULIZA: “Kwa nini hupigi saluti mbele ya bendera au kuimba wimbo wa taifa?”

      • Wewe ungejibuje?

      MUHTASARI

      Wakristo hujitahidi sana kutounga mkono upande wowote wa kisiasa kwa mawazo, maneno, na matendo yao.

      Ungejibuje?

      • Tunapaswa kuwa na maoni gani kuhusu serikali za wanadamu?

      • Kwa nini hatuungi mkono upande wowote wa kisiasa?

      • Ni hali gani zinazoweza kufanya iwe vigumu kutounga mkono upande wowote?

      Lengo

      CHUNGUZA ZAIDI

      Huenda tukahitaji kudhabihu mambo gani ili tusiunge mkono upande wowote?

      Yehova Hajatuacha Kamwe (3:14)

      Familia zinaweza kufanya nini ili kujitayarisha mapema kwa ajili ya hali zinazoweza kujaribu msimamo wao wa kutounga mkono upande wowote?

      Dumisha Msimamo wa Kutounga Mkono Upande Wowote Katika Sherehe za Umma (4:25)

      Kwa nini kutetea nchi sio heshima kubwa zaidi ambayo mtu anaweza kupata?

      “Mambo Yote Yanawezekana na Mungu” (5:19)

      Chunguza jinsi ya kutokuwa sehemu ya ulimwengu unapofanya maamuzi kuhusu kazi.

      “Kila Mmoja Ataubeba Mzigo Wake Mwenyewe” (Mnara wa Mlinzi, Machi 15, 2006)

  • Unaweza Kuvumilia Mateso
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
    • 5. Endelea kumwabudu Yehova licha ya kuteswa

      Tunahitaji ujasiri ili kumtumikia Yehova watu wengine wanapojaribu kutuzuia kumtumikia. Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali linalofuata.

      VIDEO: Kuonyesha Ujasiri Licha ya Mnyanyaso (6:27)

      • Mfano uliowekwa na akina ndugu na dada katika video hiyo unakuimarishaje?

      Soma Matendo 5:27-29 na Waebrania 10:24, 25. Baada ya kusoma kila andiko, zungumzieni swali hili:

      • Kwa nini ni muhimu sana kuendelea kumwabudu Yehova hata ikiwa serikali inatuzuia kuhubiri au kuhudhuria mikutano?

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki