-
Kuheshimu Mamlaka Ni kwa Maana Kabisa kwa Maisha Yenye AmaniAmani na Usalama wa Kweli—Wewe Unaweza Kuupataje?
-
-
11, 12. (a) Maandiko yanaonyeshaje kwamba kuna mamlaka nyingine inayopaswa kufikiriwa? (b) Wewe ungefanyaje kama watawala wa kilimwengu wangetoa maagizo yenye kupingana na matakwa ya Mungu, na kwa sababu gani?
11 Hata hivyo, Yesu alionyesha kwamba “Kaisari,” serikali ya kilimwengu, haikuwa ndiyo mamlaka ya pekee ya kufikiriwa. “Mamlaka zilizo kuu” si kuu kuliko Mungu wala hata hazilingani naye. Tofauti na hivyo, zina cheo kidogo sana kwa kulinganishwa naye. Kwa hiyo uwezo wazo una mipaka, si kamili. Kwa sababu hiyo, mara nyingi Wakristo wamekabiliwa na uamuzi mgumu. Ni uamuzi ambao lazima nawe pia uelekeane nao. Wakati ambao wanadamu wenye uwezo wanapojidaia kilicho cha Mungu, wewe utafanya nini? Wakikataza jambo linaloamriwa na Mungu, wewe utamtii nani?
12 Mitume wa Yesu walieleza msimamo wao kwa heshima lakini kwa uthabiti kwa kuwaambia washiriki wa mahakama kuu katika Yerusalemu: “Sisi hatuwezi kuacha kusema juu ya mambo ambayo tumeona na kusikia. . . . Ni lazima sisi tutii Mungu kuwa mtawala kuliko wanadamu.” (Matendo 4:19, 20; 5:29, NW) Nyakati nyingine serikali zimeweka vizuizi nyakati za dharura, na hiyo inaeleweka. Lakini nyakati nyingine vizuizi vya kiserikali huenda vikafanyizwa ili kuvuruga ibada yetu kwa Mungu na kufanya isiwezekane kutimiza wajibu mbalimbali tuliopewa na Mungu. Iweje basi? Neno la Mungu lililoongozwa na roho linajibu: “Lazima sisi tutii Mungu kuwa mtawala kuliko wanadamu.”
13, 14. (a) Imetupasa tuwe waangalifu kadiri gani tusije tukakosa kutii sheria za kilimwengu kwa sababu za kibinafsi tu? (b) Onyesha sababu za hili kutokana na Maandiko.
13 Ingawa kuheshimu wajibu huo kwa Mungu huenda kukapingana na yale ambayo “Kaisari” anataka, kufanya hivyo ni tofauti na kuvunja kwa njia ya kujitegemea sheria tusizokubaliana nazo. Ni kweli kwamba huenda sheria fulani zikaelekea kuwa zisizohitajiwa au zenye kuzuia mno, kulingana na maoni ya kibinafsi. Lakini hiyo haimpi mtu haki ya kupuuza sheria zisizopingana na sheria za Mungu. Matokeo yangekuwa nini kama watu wote wangetii sheria zile tu walizozifikiria kuwa zenye kuwafaidi wao wenyewe? Jambo hilo lingeweza kuleta machafuko ya utawala.
-
-
Kuheshimu Mamlaka Ni kwa Maana Kabisa kwa Maisha Yenye AmaniAmani na Usalama wa Kweli—Wewe Unaweza Kuupataje?
-
-
[Picha katika ukurasa wa 134]
Mitume wa Yesu waliambia mahakama kuu: “Ni lazima sisi tutii Mungu kuwa mtawala kuliko wanadamu”
-