-
Kutangaza “Habari Njema Kumhusu Yesu”“Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
-
-
3. (a) Filipo alikuwa nani? (b) Kwa nini Samaria haikuwa imehubiriwa sana, na Yesu alitabiri nini kuhusu eneo hilo?
3 Filipo ni mmoja wa “wale waliotawanyika.”a (Mdo. 8:4; ona sanduku “Filipo ‘Mweneza-Injili,’”) Alienda Samaria, jiji ambalo halikuwa limehubiriwa sana kwa sababu wakati fulani Yesu aliwaagiza mitume hivi: “Msiingie katika jiji lolote la Wasamaria; badala yake, nendeni kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.” (Mt. 10:5, 6) Hata hivyo, Yesu alijua kwamba baada ya muda fulani ushahidi kamili ungetolewa Samaria, kwa sababu kabla ya kurudi mbinguni, alisema: “Mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, katika Yudea yote na Samaria, na mpaka sehemu ya mbali zaidi ya dunia.”—Mdo. 1:8.
-
-
Kutangaza “Habari Njema Kumhusu Yesu”“Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
-
-
a Filipo huyu si mtume Filipo. Badala yake, ni Filipo ambaye, kama Sura ya 5 ya kitabu hiki inavyoeleza, alikuwa mmoja wa “wanaume saba wenye sifa nzuri” ambao waliwekwa rasmi kusimamia ugawaji wa kila siku wa chakula kati ya Wakristo wajane waliozungumza Kigiriki na waliozungumza Kiebrania katika jiji la Yerusalemu.—Mdo. 6:1-6.
-