Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Mtakuwa Mashahidi Wangu”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
    • 14, 15. (a) Malaika walisema Kristo atarudi jinsi gani, nao walimaanisha nini? (Ona pia maelezo ya chini.) (b) Ni katika maana gani Kristo alirudi “vivyo hivyo” alivyoondoka?

      14 Kama ilivyotajwa mwanzoni mwa sura hii, Yesu alipokuwa akipaa kuelekea mbinguni, mitume wake 11 walibaki wakiwa wamesimama huku wakikaza macho yao kuelekea mbinguni. Mwishowe, malaika wawili wakatokea na kuwashauri hivi kwa fadhili: “Wanaume wa Galilaya, kwa nini mnasimama mkitazama angani? Huyu Yesu aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda angani atakuja vivyo hivyo kama vile ambavyo mmemwona akienda angani.” (Mdo. 1:11) Je, walimaanisha kwamba Yesu angerudi katika mwili uleule kama vile viongozi fulani wa dini wanavyofundisha? Hapana. Tunajuaje?

      15 Malaika hao hawakusema kwamba Yesu angerudi katika umbo au mwili uleule, bali kwamba angerudi “vivyo hivyo,” au kwa njia hiyohiyo.b Aliondoka jinsi gani? Tayari alikuwa amefunikwa na mawingu malaika hao walipokuwa wakizungumza. Ni watu wachache tu, yaani mitume, ndio waliojua kwamba Yesu ameondoka duniani na kurudi mbinguni kwa Baba yake. Kristo angerudi vivyo hivyo. Na ndivyo alivyorudi. Leo, ni wale tu walio na utambuzi wa kiroho ndio wanaotambua kwamba Yesu amerudi katika maana ya kwamba sasa anatawala. (Luka 17:20) Tunahitaji kuwa macho ili kuona mambo mbalimbali yanayothibitisha kuwapo kwake na kuwaeleza wengine ili wao pia watambue kwamba mwisho unakaribia sana.

  • “Mtakuwa Mashahidi Wangu”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
    • b Biblia inatumia neno la Kigiriki troʹpos, linalomaanisha “jinsi,” bali si neno mor·pheʹ, linalomaanisha “umbo.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki