-
“Kujawa na Shangwe na Roho Takatifu”“Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
-
-
5. Eleza jinsi kisiwa cha Kipro kilivyohubiriwa.
5 Baada ya kutembea hadi Seleukia, bandari iliyokuwa karibu na Antiokia, Barnaba na Sauli walisafiri kwa mashua hadi kisiwa cha Kipro, umbali wa kilomita 200 hivi.d Kwa kuwa alikuwa mzaliwa wa Kipro, bila shaka Barnaba alikuwa na hamu kubwa ya kutangaza habari njema katika eneo la nyumbani kwao. Walipofika Salami, jiji lililokuwa kwenye ufuo wa mashariki wa kisiwa hicho, wanaume hao hawakupoteza wakati wowote. Mara moja, “wakaanza kulitangaza neno la Mungu katika masinagogi ya Wayahudi.”e (Mdo. 13:5) Barnaba na Sauli walisafiri kutoka upande mmoja hadi upande wa pili wa Kipro, wakihubiri katika majiji makubwa yaliyokuwa njiani. Ikitegemea barabara waliyopitia, huenda wamishonari hao walitembea kilomita 160 hivi!
-
-
“Kujawa na Shangwe na Roho Takatifu”“Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
-
-
d Katika karne ya kwanza, meli zingeweza kusafiri kilomita 150 hivi kwa siku ikitegemea upepo. Safari hiyo ingechukua muda mrefu zaidi ikiwa hali ya hewa ni mbaya.
-