-
“Kujawa na Shangwe na Roho Takatifu”“Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
-
-
6, 7. (a) Sergio Paulo ni nani, na kwa nini Bar-Yesu alijaribu kumzuia asisikilize habari njema? (b) Sauli alishughulikiaje upinzani wa Bar-Yesu?
6 Katika karne ya kwanza, ibada ya uwongo ilikuwa imeenea sana Kipro. Hilo lilionekana wazi Barnaba na Sauli walipofika Pafo, kwenye ufuo wa magharibi wa kisiwa hicho. Huko walikutana “na mwanamume Myahudi aliyeitwa Bar-Yesu, ambaye alikuwa mlozi na nabii wa uwongo, [naye] alikuwa pamoja na liwali Sergio Paulo, mwanamume mwenye akili.”f Katika karne ya kwanza, Waroma wengi wenye kuheshimika—hata ‘wanaume wenye akili,’ kama Sergio Paulo—waliwaendea walozi au wanajimu kutafuta msaada wa kufanya maamuzi mazito. Hata hivyo, Sergio Paulo alivutiwa sana na ujumbe wa Ufalme naye “alitamani kulisikia neno la Mungu.” Hilo halikumpendeza Bar-Yesu, ambaye jina lake la cheo lilikuwa Elima, yaani, “Mlozi.”—Mdo. 13:6-8.
-
-
“Kujawa na Shangwe na Roho Takatifu”“Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
-
-
f Kisiwa cha Kipro kilikuwa chini ya utawala wa Roma. Mkuu wa kisiwa hicho alikuwa liwali.
-