Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Tafuta Wenye Mwelekeo Unaofaa Kwa Ajili ya Uhai wa Milele
    Mnara wa Mlinzi—1991 | Januari 15
    • 2. Ni nini kimetia mizizi katika moyo wa kitamathali wa mtu, na hivyo twasoma nini juu ya hili katika Maandiko?

      2 Mtu huonyesha mwelekeo fulani mkuu. Yeye huwa na nia fulani hasa ambayo imetia mizizi katika moyo wake wa kitamathali. (Mathayo 12:34, 35; 15:18-20) Hivyo, twasoma juu ya mtu ambaye “moyo wake ni vita [una mwelekeo wa kupigana, NW].” (Zaburi 55:21) Twaambiwa kwamba “mtu mwenye ghadhabu huasi sana [ana makosa mengi, NW].” Na twasoma hivi: “Kuna marafiki wenye mwelekeo wa kuvunjana vipande vipande, lakini kuna rafiki anayeshikamana kwa ukaribu sana kuliko ndugu.” (Mithali 18:24, NW; 29:22, UV) Kwa furaha, wengi wanathibitika kuwa kama watu fulani wasio Wayahudi katika Antiokia ya kale katika Pisidia. Waliposikia juu ya uandalizi wa Yehova kwa ajili ya wokovu, “walianza kushangilia na kutukuza lile neno la Yehova, na wote wale waliokuwa na mwelekeo wenye kufaa kwa ajili ya uhai wa milele wakawa waamini.”—Matendo 13:44-48, NW.

  • Tafuta Wenye Mwelekeo Unaofaa Kwa Ajili ya Uhai wa Milele
    Mnara wa Mlinzi—1991 | Januari 15
    • 4 Wenye moyo safi ni safi kwa ndani. Usafi wa uthamini, wa shauku, tamaa, na wa makusudio ni wao. (1 Timotheo 1:5) Wao wamwona Mungu sasa kwa njia ya kwamba wamwona akitenda kwa ajili ya washikao ukamilifu wa kimaadili. (Linganisha Kutoka 33:20; Ayubu 19:26; 42:5.) Neno la Kigiriki lililofasiriwa hapa ‘ona’ linamaanisha pia ‘kuona kwa akili, kuhisi, kujua.” Kwa kuwa Yesu alionyesha kikamilifu utu wa Mungu, kuwa na muono-ndani katika utu huo kunaonewa shangwe na “wenye moyo safi,” ambao hujizoeza imani katika Kristo na katika dhabihu yake yenye kulipia dhambi, hupata msamaha wa dhambi zao, na waweza kutolea Mungu ibada yenye kukubalika. (Yohana 14:7-9; Waefeso 1:7) Kwa wapakwa mafuta, kumwona Mungu hufikia kilele wafufuliwapo kwenda mbinguni, ambako kwa kweli wao huona Mungu na Kristo. (2 Wakorintho 1:21, 22; 1 Yohana 3:2) Lakini kuona Mungu kupitia maarifa sahihi na ibada ya kweli kwawezekana kwa wote wale wenye moyo safi. (Zaburi 24:3, 4; 1 Yohana 3:6; 3 Yohana 11) Wao wana mwelekeo unaofaa kwa ajili ya uhai wa milele mbinguni au katika dunia-paradiso.—Luka 23:43; 1 Wakorintho 15:50-57; 1 Petro 1:3-5.

      5. Ni jinsi gani tu mtu aweza kuwa mwaminifu na mfuasi wa kweli wa Yesu Kristo?

      5 Wale wasio na mwelekeo unaofaa kwa ajili ya uhai wa milele hawatakuwa waamini. Haiwezekani kwao kujizoeza imani. (2 Wathesalonike 3:2) Zaidi ya hilo, hakuna mtu awezaye kuwa mfuasi wa kweli wa Yesu Kristo iwapo yeye si mwenye kufundishika, na Yehova ambaye huona moyo ulivyo humvuta mtu huyo. (Yohana 6:41-47) Bila shaka, katika kuhubiri kutoka nyumba kwa nyumba, Mashahidi wa Yehova hawatangulii kuhukumu mtu yeyote. Hawawezi kusoma mioyo bali wao huacha matokeo katika mikono ya Mungu yenye upendo.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki