Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Anaijaza ‘Mioyo Yetu Kikamili’
    Mnara wa Mlinzi—2013 | Julai 1
    • Je, kweli Mungu anatujali, au je, anaona mateso yanayowapata wanadamu? Biblia inajibu swali hilo kwa njia yenye kuridhisha. Bila shaka, Mungu anawajali wanadamu, na anataka wafurahie maisha. Kila siku anawaruhusu wanadamu kutia ndani wale wasio na shukrani wafaidike na wema wake mwingi. Acheni tuchunguze maneno ya mtume Paulo.​—Soma Matendo 14:16, 17.

      Alipokuwa akihutubia watu wa jiji la Listra ambao hawakuwa waabudu wa Mungu, Paulo alisema hivi: “Katika vizazi vilivyopita [Mungu] aliwaruhusu mataifa yote waendelee kutembea katika njia zao, ijapokuwa, kwa kweli, hakujiacha mwenyewe bila ushahidi kwa kuwa alitenda mema, akiwapa ninyi mvua kutoka mbinguni na majira yenye kuzaa matunda, akijaza mioyo yenu kikamili kwa chakula na uchangamfu.” Maneno hayo yalimaanisha nini kwa wasikilizaji wa Paulo?

  • Anaijaza ‘Mioyo Yetu Kikamili’
    Mnara wa Mlinzi—2013 | Julai 1
    • Yehova anaturuhusu tujiamulie mambo. Ona kwamba Yehova aliruhusu watu wa mataifa yote “waendelee kutembea katika njia zao.” Kitabu kimoja cha marejezo ya Biblia kinasema maneno hayo yanaweza kumaanisha “kutembea kama walivyopenda” au “kufanya kulingana na mapendezi yao.” Yehova hamlazimishi mtu yeyote amwabudu. Ametupatia hiari, yaani, uwezo wa kuamua jinsi tutakavyoishi.​—Kumbukumbu la Torati 30:19.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki