Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Wakizungumza kwa Ujasiri kwa Mamlaka ya Yehova”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
    • Paulo na Barnaba wakikataa kusifiwa na umati jijini Listra. Watu hao wanacheza muziki, wanatayarisha dhabihu na kuinama mbele yao.

      “Mgeuke kutoka katika mambo haya ya bure mje kwa Mungu aliye hai, aliyeumba mbingu na dunia.”—Matendo 14:15

      11-13. (a) Paulo na Barnaba waliwaambia nini wenyeji wa Listra? (b) Tunaweza kujifunza nini kutokana na maneno ya Paulo na Barnaba?

      11 Licha ya mambo hayo yote, Paulo na Barnaba walijitahidi kufikia mioyo ya wasikilizaji wao kwa njia bora zaidi. Katika kisa hiki, Luka anaeleza njia yenye mafanikio iliyotumiwa kuwahubiria wapagani habari njema. Ona jinsi Paulo na Barnaba walivyowasihi wasikilizaji wao: “Wanaume, kwa nini mnafanya mambo haya? Sisi pia ni wanadamu tulio na udhaifu kama wenu. Nasi tunawatangazia habari njema, ili mgeuke kutoka katika mambo haya ya bure mje kwa Mungu aliye hai, aliyeumba mbingu na dunia na bahari na vitu vyote vilivyomo. Katika vizazi vilivyopita aliruhusu watu wa mataifa yote waendelee kutembea katika njia zao, ingawa hakujiacha bila ushahidi kwa kuwa alitenda mema, akiwapa ninyi mvua kutoka mbinguni na majira ya mavuno, akiwashibisha kwa chakula na kuijaza mioyo yenu furaha.”​—Mdo. 14:15-17.

  • “Wakizungumza kwa Ujasiri kwa Mamlaka ya Yehova”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
    • 14-16. Ni masomo gani mengine tunayojifunza kutokana na mambo ambayo Paulo na Barnaba waliwaambia watu wa Listra?

      14 Jambo la pili tunaloweza kujifunza kutokana na mazungumzo hayo ni; Paulo na Barnaba walibadilika kulingana na hali. Wayahudi na wageuzwa imani waliokuwa Ikoniamu walijua mengi kuhusu Maandiko au jinsi Mungu alivyoshughulika na taifa la Israeli, lakini watu wa Listra walijua mambo machache au hawakujua kabisa mambo hayo. Hata hivyo, wale waliowasikiliza Paulo na Barnaba walikuwa wakulima. Jiji la Listra lilikuwa na hali nzuri ya hewa na mashamba yenye rutuba. Watu hao wangeweza kuona uthibitisho wa kutosha wa sifa za Muumba kupitia mambo kama vile majira ya mavuno, na wamishonari hao walitumia jambo hilo kama msingi wa kuwahubiria.​—Rom. 1:19, 20.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki