-
Kupatana Katika UpendoUnaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
-
-
8. (a) Ni matata gani yaliyotokea kati ya Paulo na Barnaba? (b) Kama ungalikuwapo ukaona matata hayo, ungalikata shauri gani?
8 Siku moja vilevile kulitokea matata kati ya mtume Paulo na msafiri mwenzake Barnaba. Walipokuwa karibu kuondoka katika safari yao ya pili ya umisionari, Barnaba alitaka achukue Marko binamu yake aende pamoja nao. Walakini, Paulo hakutaka Marko aandamane nao, kwa vile Marko alivyokuwa amewaacha akarudi nyumbani wakati wa safari yao ya kwanza ya umisionari. (Matendo 13:13) Biblia inasema: “Ndipo kukatokea mfoko mkali wa hasira, hivi kwamba wakatengana mmoja na mwenzake.” (Matendo 15:37-40, NW) Ebu wazia hilo! Kama ungalikuwapo na kuona huo “mfoko mkali wa hasira,” je! ungalikata shauri kwamba Paulo na Barnaba hawakuwa sehemu ya tengenezo la Mungu kwa sababu ya mwenendo waliouonyesha wakati huo?
-
-
Kupatana Katika UpendoUnaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
-
-
11. (a) Ijapokuwa walifanya mfoko wa hasira, Paulo na Barnaba walionyeshaje kwamba walikuwa Wakristo wa kweli? (b) Tunaweza kufaidikaje na mfano wao?
11 Namna gani lile tatizo lililokuwa kati ya Paulo na Barnaba? Hilo pia lilimalizwa kwa upendo. Kwa maana baadaye, Paulo alipoliandikia kundi la Korintho, alimtaja Barnaba kuwa mfanya kazi mwenzake aliye mkubwa sana. (1 Wakorintho 9:5, 6) Ijapokuwa Paulo anaonekana kuwa alikuwa na sababu nzuri ya kutilia mashaka ubora wa Marko kama mwenzi wa kusafiri nao, baadaye kijana huyo alikomaa kwa kiasi cha kwamba Paulo aliweza kumwandikia Timotheo hivi: “Umtwae Marko, umlete pamoja nawe, maana anifaa kwa utumishi.” (2 Timotheo 4:11) Tunaweza kufaidika na mfano huo wa kumaliza tofauti kati ya mtu na mwenzake.
-