-
Fanya Mambo Yote kwa Ajili ya Habari NjemaMnara wa Mlinzi—1989 | Novemba 15
-
-
3. Nia ya Paulo kufanya mambo yote kwa ajili ya habari njema ilionyeshwaje kuhusiana na Timotheo na Wayahudi?
3 Malezi ya Kiyahudi ya Paulo na nia yake ya kufanya mambo yote kwa ajili ya habari njema yalimwandaa kusaidia Wayahudi wanyenyekevu wamkubali Yesu kuwa ndiye Mesiya. Kwa kielelezo, fikiria alilofanya mtume wakati alipochagua Timotheo awe mwandamani wake mwenye kusafiri. Timotheo, ambaye baba yake alikuwa Mgiriki, hakuwa ametahiriwa kama vile watoto waume wa Kiyahudi walivyokuwa wamefanywa. (Walawi 12:2, 3) Paulo alijua kwamba Wayahudi wangeweza kukwazwa ikiwa kijana mwana-mume asiyetahiriwa angejaribu kuwasaidia wapatanishwe na Mungu. Kwa hiyo, ili Wayahudi wenye mioyo ya kufuata haki wasiweze kuwa na kizuizi cha kutokubali Yesu, Paulo alifanya nini? “Alimchukua [Timotheo] na kumtahiri kwa sababu ya Wayahudi.” Jambo hili lilifanywa hata ingawa tohara haikuwa takwa la Kikristo.—Matendo 16:1-3, NW.
4. Kulingana na 1 Wakorintho 9:20, lengo la Paulo lilikuwa nini?
4 Basi Paulo alikuwa akifanya mambo kwa ajili ya habari njema alipoonyesha hangaiko lenye upendo kwa Wayahudi wenzake. Aliandika hivi: “Nalikuwa kama Myahudi kwa Wayahudi, ili niwapate Wayahudi; kwa wale walio chini ya sheria, nalikuwa kama chini ya sheria, (ingawa mimi mwenyewe si chini ya sheria,) ili niwapate walio chini ya sheria.” (1 Wakorintho 9:20) Ndiyo, kama vile kisa cha Timotheo kitoavyo kielezi, Paulo alifanya yale ambayo angeweza ili awapate Wayahudi, kuwasaidia wawe Wakristo. Lakini je! alishughulika jinsi iyo hiyo pamoja na Wasio Wayahudi?
-
-
Fanya Mambo Yote kwa Ajili ya Habari NjemaMnara wa Mlinzi—1989 | Novemba 15
-
-
7. Kuhusu tohara, kwa nini hali ya Tito ilitofautiana na ile ya Timotheo?
7 Paulo alipoenda Yerusalemu karibu 49 W.K. ili kuhudhuria mkutano wa maana wa baraza lenye kuongoza la kundi la Kikristo, aliandamwa na Tito mwanafunzi Mgiriki. Paulo aliwatolea ndugu waliokusanyika ripoti fulani kuhusu kazi yake ya kuhubiri miongoni mwa mataifa, na baadaye akaandika hivi: “Wala hata Tito, aliyekuwa pamoja nami, hakushurutika kutahiriwa, ingawa alikuwa ni Mgiriki.” (Wagalatia 2:1-3, NW) Tofauti na Timotheo, Tito alifanya huduma yake miongoni mwa watu wa mataifa wasiotahiriwa hasa. Kwa sababu hiyo, suala la tohara halikutokea katika kisa chake. —2 Wakorintho 8:6, 16-18, 23; 12:18; Tito 1:4, 5.
-