Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Jifunze Jinsi ya Kukesha Kutoka kwa Mitume wa Yesu
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Januari 15
    • 4, 5. Roho takatifu ilimwongozaje Paulo na wasafiri wenzake?

      4 Somo la kwanza ni kwamba mitume walikuwa macho ili kuona jinsi ambavyo wangeelekezwa mahali pa kuhubiri. Simulizi moja la Biblia linaonyesha jinsi Yesu alivyotumia roho takatifu aliyopewa na Yehova ili kumwongoza mtume Paulo na wasafiri wenzake katika safari isiyo ya kawaida. (Mdo. 2:33) Acheni tujiunge nao.​—Soma Matendo 16:6-10.

  • Jifunze Jinsi ya Kukesha Kutoka kwa Mitume wa Yesu
    Mnara wa Mlinzi—2012 | Januari 15
    • 7 Kufikia hapo, wanaume hao walifanya uamuzi ambao unaweza kuonwa kuwa usio wa kawaida. Mstari wa 8 unatuambia hivi: “Wakapita Misia na kushuka mpaka Troa.” Hivyo, wasafiri hao walielekea magharibi na wakatembea kilomita 563, huku wakipita jiji baada ya jiji hadi walipofika kwenye bandari ya Troa, ambayo kutoka hapo watu walisafiri kwenda Makedonia kwa meli. Wakiwa huko, kwa mara ya tatu, Paulo na wenzake walibisha mlango, lakini mara hii mlango ulifunguliwa wazi! Mstari wa 9 unatuambia mambo yaliyotukia baadaye: “Usiku maono yakamtokea Paulo: mwanamume fulani Mmakedonia alikuwa amesimama akimsihi na kusema: ‘Vuka uingie Makedonia utusaidie.’” Hatimaye, Paulo alijua ni wapi wangehubiri. Bila kukawia, wanaume hao walisafiri kwa meli kwenda Makedonia.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki