-
Via Egnatia—Barabara Kuu Iliyosaidia Kuleta MpanukoAmkeni!—1997 | Agosti 22
-
-
Msaada mkubwa sana katika kueneza Ukristo katika Makedonia ulikuwa Via Egnatia, barabara kuu ya Roma iliyotengenezwa. Baada ya kutua kwenye bandari ya Neapolisi (sasa Kaválla, Ugiriki) mwisho wa kaskazini mwa Bahari ya Aegean, wamishonari hao kwa wazi walisafiri kwenye barabara kuu hiyo hadi Filipi, jiji kuu la wilaya ya Makedonia. Barabara hiyo iliendelea hadi Amfipolisi, Apolonia, na Thesalonike, zilizokuwa sehemu ambazo Paulo angetua pamoja na waandamani wake.—Matendo 16:11–17:1.
-
-
Via Egnatia—Barabara Kuu Iliyosaidia Kuleta MpanukoAmkeni!—1997 | Agosti 22
-
-
Kutoka Filipi, Paulo na washiriki wake waliendelea kwenye Via Egnatia kupitia Amfipolisi na Apolonia hadi Thesalonike, jumla ya kilometa 120. (Matendo 17:1) Ili kuhubiri habari njema katika Thesalonike, Paulo alitumia vikusanyiko vya Wayahudi vya siku ya Sabato katika sinagogi la huko. Kwa hiyo, Wayahudi fulani na “umati mkubwa kati ya Wagiriki” wakawa waamini.—Matendo 17:2-4.
-