-
Kupambana Sana kwa Ajili ya Habari Njema Huko ThesalonikeMnara wa Mlinzi—2012 | Juni 1
-
-
Kwa kawaida Paulo alipofika katika jiji, alikuwa akianza kuzungumza na Wayahudi kwa sababu walifahamu Maandiko na hivyo angeweza kuyatumia katika mazungumzo yake na kuwasaidia kuelewa habari njema. Msomi fulani anadokeza kwamba huenda Paulo alifanya hivyo kwa kuwa aliwajali sana watu wa nchi yake au alitaka kuwatumia Wayahudi na watu waliomwogopa Mungu ili kuanza kazi yake ya kuwafikia Watu wa Mataifa.—Matendo 17:2-4.
Hivyo alipofika Thesalonike, Paulo aliingia katika sinagogi, na “akajadiliana nao [Wayahudi] kwa kutumia Maandiko, akieleza na kuthibitisha kwa marejeo kwamba ilikuwa lazima Kristo ateseke na kufufuliwa kutoka kwa wafu, akisema: ‘Huyu ndiye Kristo, Yesu huyu ninayewatangazia ninyi.’”—Matendo 17:2, 3, 10.
Jambo ambalo Paulo alizungumzia, yaani, daraka la Masihi na utambulisho wake, lilikuwa jambo lililokuwa likibishaniwa. Wayahudi walitazamia Masihi ambaye angewakomboa kutoka kwa utawala wa Waroma, hivyo kuteseka kwa Masihi kulikuwa kinyume cha matarajio yao. Ili afaulu kuwashawishi Wayahudi, Paulo ‘alijadiliana,’ ‘akaeleza,’ na ‘kuthibitisha kwa kurejelea’ Maandiko—mbinu inayotumiwa na mwalimu mwenye ustadi.a Lakini wasikilizaji wa Paulo waliitikiaje alipokuwa akiwafundisha mambo hayo mazuri?
-
-
Kupambana Sana kwa Ajili ya Habari Njema Huko ThesalonikeMnara wa Mlinzi—2012 | Juni 1
-
-
a Huenda Paulo alirejelea maandiko ambayo sasa yanajulikana kama Zaburi 22:7; 69:21; Isaya 50:6; 53:2-7; na Danieli 9:26.
-