-
Je! Wewe Una Akili Iliyofunguka Kupokea Mawazo Mapya?Mnara wa Mlinzi—1989 | Januari 15
-
-
Hata hivyo, walikuwako watu wenye nia ya kutazama ng’ambo ya maoni yao ya kuhukumu kabla ya uchunguzi. Mathalani, wakaaji wa Beroya waliitikiaje habari njema zilizohubiriwa na mtume Paulo na Sila mshirika wake? Kuhusu Waberoya, Luka mwandikaji wa Biblia alisema hivi: “Watu hawa walikuwa waungwana [washarifu katika akili, JVW] kuliko wale wa Thesalonike, kwa kuwa walilipokea lile neno kwa uelekevu wa moyo, wakayachunguza maandiko kila siku, waone kwamba mambo hayo ndivyo yalivyo.” (Matendo 17:11) Je! wewe ni ‘msharifu katika akili’ kama Waberoya?
Tafadhali fikiria kisa cha Masaji. Wakati mmoja, yeye alikuwa na uhasama mkali kuelekea Ukristo. Alikuwa kama wale watu wenye kujitenga waliopinga Japani isifunguliwe wazi. Mke wake, Sachiko, alipoanza kujifunza Biblia, mume huyo alimpinga kijeuri. Hata alifikiria kuua jamaa yake kisha ajiue mwenyewe. Kwa sababu ya jeuri yake, jamaa yake ililazimika kukimbilia maskani ya ndugu mkubwa wa Sachiko kaskazini mwa Japani.
Mwishowe, Masaji aliamua kufungua kidogo akili yake na kuchunguza dini ya mke wake. Baada ya kusoma fasihi fulani ya Biblia, aliona uhitaji wa kufanya mabadiliko. Alipokuwa akijifunza Maandiko, mwelekeo wake wenye jeuri ulibadilika ukawa wa kuonyesha tunda la roho ya Mungu. (Wagalatia 5:22, 23) Masaji alisitasita kuhudhuria mikutano ya Mashahidi wa Yehova kwa sababu alihofu kwamba Mashahidi wangeweza kutafuta kisasi kwa sababu ya jeuri aliyofanya dhidi yao. Lakini mwishowe alipozuru Jumba la Ufalme, alikaribishwa kwa uchangamfu mwingi sana hata akabubujisha machozi.
-
-
Je! Wewe Una Akili Iliyofunguka Kupokea Mawazo Mapya?Mnara wa Mlinzi—1989 | Januari 15
-
-
Tunaweza kujifunza nini kutokana na hilo? Kwamba inatupasa kuwa wachaguzi katika kukubali mawazo mapya. Ingefaa tuige Waberoya ‘walioyachunguza maandiko kila siku, waone kwamba mambo hayo [yaliyofunzwa na Paulo] ndivyo yalivyo.” (Matendo 17:11) Neno la Kigiriki ambalo hapa limetafsiriwa ‘kuchunguza’ linamaanisha ‘kufanya utafiti wa uangalifu na wa kufuata mambo kama yalivyo hasa kama vile inavyokuwa katika taratibu za kuchunguza mambo ya kisheria.” (Word, Pictures in the New Testament, kilichotungwa na A. T. Robertson) Badala ya kukubali kwa upofu kila wazo jipya tunalotokezewa, tunahitaji kufanya utafiti wa uangalifu na wa kufuata mambo kama yalivyo hasa, sawa na vile hakimu angefanya katika kusikia kesi ya kisheria.
-