Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Wakajazwa Roho Takatifu”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
  • “Wakajazwa Roho Takatifu”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” Kuhusu Ufalme wa Mungu
    • Kati ya watu waliosikiliza hotuba ya Petro siku ya Pentekoste ya mwaka wa 33 W.K. walikuwa Wayahudi kutoka Ponto, wilaya iliyo kaskazini mwa Asia Ndogo. (Mdo. 2:9) Kwa kuwa wale ambao Petro aliwatumia barua yake ya kwanza walitia ndani waamini “waliotawanyika” katika mkoa wa Ponto, inaonekana kwamba baadhi ya Wayahudi walirudi na habari njema nyumbani kwao.g (1  Pet. 1:1) Aliandika kwamba Wakristo hao walikuwa ‘wamehuzunishwa kwa majaribu ya namna mbalimbali’ kwa sababu ya imani yao. (1 Pet. 1:6) Huenda majaribu hayo yalitia ndani upinzani na mateso.

      Majaribu mengine yaliyowapata Wakristo huko Ponto yanarejelewa kwa njia isiyo ya moja kwa moja katika mawasiliano kati ya Plini Mdogo, aliyekuwa gavana wa jimbo la Bithinia na Ponto, na Maliki Trajani. Akiandika kutoka Ponto karibu mwaka wa 112 W.K., Plini alisema kwamba kila mtu, haidhuru jinsia yake, umri wake, au cheo chake angeweza “kuambukizwa” Ukristo. Plini aliwapa wale waliokuwa Wakristo nafasi ya kukana imani yao la sivyo, wauawe. Yeyote aliyemlaani Kristo au kusali kwa miungu au kwa sanamu ya Trajani, aliachiliwa huru. Plini alikiri kwamba hayo ni mambo ambayo “Wakristo wa kweli hawangeweza kufanya.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki