Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Dhihirisha Shauku ya Kuzitangaza Habari Njema
    Mnara wa Mlinzi—1987 | Februari 1
    • 9. Paulo alidhihirishaje shauku ya kuzitangaza habari njema?

      9 Hata hivyo, Paulo hakuhisi kwamba alikuwa na mambo ya kutosha ya kufanya, wala yeye hakusababu (hakutoa sababu) ya kwamba alikuwa na mgawo wa kufanya hayo na yalikuwa mambo tele. Yeye alitaka kufanya zaidi. Kwa kweli, yeye alisema: “Kunabaki kwa upande wangu kuzitangaza habari njema kwenu pia huko katika Rumi.” Hivyo ndivyo hasa mtu mwenye shauku anavyokuwa! Kwa kufaa, Profesa F. F. Bruce katika kitabu chake The Epistle of Paul to the Romans alisema hivi juu ya mtume huyo: “Kuhubiri injili kumo katika damu yake, naye hawezi kujiepusha nako; kwake yeye hakuna siku inaposemwa kwamba ‘leo ilikuwa siku yake ya kutokuja kazini,’ bali analazimika kuifanya daima akizidisha kidogo-kidogo kulipa deni alilo nalo kwa wanadamu wote—deni ambalo hakuna siku atakapoweza kulilipa kwa ukamili maadamu yuko hai.” Je! hivyo ndivyo wewe unavyoiona huduma?

  • Dhihirisha Shauku ya Kuzitangaza Habari Njema
    Mnara wa Mlinzi—1987 | Februari 1
    • “Mdeni” kwa Wote

      11. Ni nini maana ya “Mimi ni mdeni”?

      11 Kulikuwa na kani nyingine yenye kusukuma jitihada za Paulo za kutokuchoka katika kuzitangaza habari njema. “Kwa wote Wagiriki na kwa Washenzi, kwa wote wenye hekima na kwa wasiotumia akili mimi ni mdeni,” akasema Paulo. (Warumi 1:14, NW) Ni kwa njia gani Paulo alikuwa “mdeni”? Tafsiri nyingine zinatafsiri neno hilo kuwa “Mimi niko chini ya wajibu” (New English Bible). “Mimi nina wajibu fulani” (Today’s English Version), au “Mimi ninawia wajibu fulani” (Jerusalem Bible). Basi je! yeye alikuwa akisema kwamba kazi ya kuhubiri ilikuwa wajibu au sharti lenye kulemea kama mzigo ambalo alipaswa kutimiza mbele za Mungu? Ni rahisi kukuza mwelekeo kama huo tukiacha kuona uharaka uliopo au tukipotoshwa fikira na vivutia-macho vya kilimwengu. Lakini hilo silo jambo ambalo Paulo alikuwa nalo akilini.

      12. Paulo alikuwa “mdeni” kwa nani, na kwa sababu gani?

      12 Akiwa “chombo kichaguliwa” cha Mungu na “mtume kwa mataifa,” Paulo alikuwa na daraka zito sana mbele za Mungu. (Matendo 9:15; Warumi 11:13, NW) Hata hivyo yeye hakuhisi wajibu wake kwa Mungu tu. Yeye alisema alikuwa “mdeni” kwa ‘Wagiriki, Washenzi, wenye hekima na wasiotumia akili yao.’ Kwa ajili ya rehema na pendeleo alilopewa, yeye alihisi ulikuwa wajibu wake kuhubiri ili kwamba watu wote wapate kuzisikia habari njema. Alitambua, pia, kwamba ni mapenzi ya Mungu “namna zote za watu waokolewe na kuja kwenye maarifa yaliyo sahihi ya ukweli.” (1 Timotheo 1:12-16; 2:3, 4, NW) Hiyo ndiyo sababu yeye alifanya kazi ya jasho kwa kurudia-rudia, si ili aishi kwa kusudi la kutimiza tu daraka lake kuelekea Mungu na basi, bali pia ili atimize deni lake kwa wanadamu wenzake. Je! wewe unahisi ukiwa na deni kama hilo la kibinafsi kuelekea watu katika eneo lenu? Je! wewe unahisi kuwa unawawia watu hao deni la kujitahidi sana uwaletee habari njema.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki