Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mungu Anapendekeza Upendo Wake Kwetu
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Juni 15
    • 7, 8. Maisha ya wanaume wawili wakamilifu yalileta jinsi gani matokeo tofauti?

      7 Kwa upendo, Mungu alifanya mpango ili wanadamu wawe huru kutokana na dhambi waliyorithi. Paulo alieleza kwamba hilo liliwezekana kupitia mwanadamu mwingine, mwanamume mkamilifu aliyeishi baadaye, yaani, Adamu wa pili. (1 Kor. 15:45) Lakini maisha ya kila mmoja wa wanaume hao wawili wakamilifu yameleta matokeo yaliyo tofauti kabisa. Jinsi gani?—Soma Waroma 5:15, 16.

      8 Paulo aliandika hivi: “Sivyo ilivyo kwa ile zawadi kama ilivyokuwa kwa lile kosa.” Adamu alikuwa na hatia ya kosa hilo, na kwa haki alipokea adhabu kali, alikufa. Hata hivyo, hangekufa peke yake. Tunasoma hivi: “Kwa kosa la mtu [huyo] mmoja wengi walikufa.” Hukumu ya haki iliyotolewa kwa Adamu ilitaka kwamba wazao wake wote wasio wakamilifu wapate adhabu hiyohiyo, kutia ndani sisi. Lakini bado tunaweza kufarijiwa kwa kujua kwamba mwanamume mkamilifu, Yesu, angeweza kuleta matokeo yaliyo kinyume kabisa. Matokeo gani? Tunapata jibu katika maneno haya ya Paulo: “Kutangazwa [kwa watu wa namna zote] kuwa waadilifu kwa ajili ya uzima.”—Rom. 5:18.

      9. Mungu alikuwa akifanya nini alipotangaza wanadamu kuwa waadilifu, kama inavyotajwa katika Waroma 5:16, 18?

      9 Ni nini maana ya maneno ya Kigiriki yanayotafsiriwa kuwa “tangazo la uadilifu” na “kutangazwa kuwa waadilifu”? Mtafsiri mmoja wa Biblia aliandika hivi kuhusu wazo hilo: “Ni maneno ya mfano ya kisheria ambayo yanaonyesha jambo halali kisheria. Yanaonyesha badiliko la msimamo wa mtu mbele za Mungu, si badiliko linalofanyika ndani ya mtu . . . Maneno hayo ya mfano yanaonyesha kwamba Mungu ni hakimu au mwamuzi ambaye amefanya uamuzi ambao unampendelea mshtakiwa, ambaye ameletwa mbele ya mahakama ya Mungu, kwa njia ya mfano, akiwa ameshtakiwa kwa kosa la kutokuwa mwadilifu. Lakini Mungu anamwondolea mshtakiwa huyo hatia.”

  • Mungu Anapendekeza Upendo Wake Kwetu
    Mnara wa Mlinzi—2011 | Juni 15
    • 14, 15. Ni thawabu gani ambayo wale wanaotangazwa na Mungu kuwa waadilifu waliahidiwa, lakini bado walihitaji kufanya nini?

      14 Hebu fikiria zawadi kubwa ajabu kutoka kwa Mweza-Yote ya kusamehe dhambi ambazo mtu alirithi kutia ndani makosa aliyofanya! Huwezi kuhesabu dhambi ambazo watu mmoja-mmoja walitenda kabla ya kuwa Wakristo; hata hivyo, kwa msingi wa dhabihu ya ukombozi, Mungu anaweza kusamehe dhambi hizo. Paulo aliandika hivi: “Zawadi ilitokana na makosa mengi katika tangazo la uadilifu.” (Rom. 5:16) Mitume na watu wengine ambao walipokea zawadi hiyo yenye upendo (kutangazwa kuwa waadilifu) walipaswa kuendelea kumwabudu Mungu wa kweli wakiwa na imani. Wangepata thawabu gani wakati ujao? ‘Wale wanaopokea wingi wa fadhili zisizostahiliwa na zawadi ya bure ya uadilifu watatawala wakiwa wafalme katika uzima kupitia mtu mmoja, Yesu Kristo.’ Kwa kweli, zawadi ya uadilifu ina matokeo yaliyo tofauti kabisa. Zawadi hiyo inatokeza uzima.—Rom. 5:17; soma Luka 22:28-30.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki