-
Tumaini la Ufufuo Ni Hakika!Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2020 | Desemba
-
-
Yesu alikuwa wa kwanza kufufuliwa kati ya wengi watakaofufuliwa kwenda mbinguni (Tazama fungu la 15 na 16)b
15. “Wote” ambao “watafanywa kuwa hai” wanatia ndani akina nani?
15 Ona kwamba Paulo alisema “katika Kristo wote watafanywa kuwa hai.” (1 Kor. 15:22) Paulo aliwaandikia barua hiyo Wakristo watiwa-mafuta huko Korintho, ambao wangefufuliwa ili wakaishi mbinguni. Wakristo hao walikuwa ‘wametakaswa katika muungano na Kristo Yesu na kuitwa kuwa watakatifu.’ Na Paulo aliwataja “wale ambao wamelala usingizi katika kifo wakiwa katika muungano na Kristo.” (1 Kor. 1:2; 15:18; 2 Kor. 5:17) Katika barua yake nyingine iliyoongozwa na roho, mtume Paulo aliandika kwamba wale ‘walioungana pamoja na Yesu katika mfano wa kifo chake wataunganishwa pamoja naye katika mfano wa ufufuo wake.’ (Rom. 6:3-5) Yesu alifufuliwa akiwa kiumbe wa roho na alienda mbinguni. Itakuwa vivyo hivyo kwa wote walio “katika muungano na Kristo,” yaani, Wakristo wote waliotiwa mafuta kwa roho.
-
-
Tumaini la Ufufuo Ni Hakika!Mnara wa Mlinzi (Funzo)—2020 | Desemba
-
-
17. Wale walio “katika muungano pamoja na Kristo” watapokea lini thawabu yao ya kimbingu?
17 Paulo alipoandika barua yake kwa Wakorintho, ufufuo wa kwenda mbinguni kwa wale walio “katika muungano na Kristo” ulikuwa bado haujaanza. Lakini Paulo alionyesha kwamba ungetukia wakati ujao: “Kila mmoja kwa mpangilio wake unaofaa: Kristo aliye matunda ya kwanza, baadaye wale walio wa Kristo wakati wa kuwapo kwake.” (1 Kor. 15:23; 1 The. 4:15, 16) Leo tunaishi katika kipindi hicho kilichotabiriwa cha “kuwapo” kwa Kristo. Naam, mitume na Wakristo wengine waliotiwa mafuta kwa roho ambao walikuwa wamekufa, walihitaji kusubiri kipindi hicho cha kuwapo kwa Kristo ili kupokea thawabu yao ya kimbingu na ‘kuunganishwa pamoja na Yesu katika mfano wa ufufuo wake.’
-