-
Tembea Kupatana na Roho ili Upate Uzima na AmaniMnara wa Mlinzi—2011 | Novemba 15
-
-
8 Sheria, pamoja na amri zake nyingi, ziliwahukumu watenda-dhambi. Zaidi ya hayo, makuhani wakuu wa Israeli waliotumika chini ya Sheria hawakuwa wakamilifu na hawangeweza kutoa dhabihu ya kufunika dhambi kikamili. Hivyo, Sheria ilikuwa “dhaifu kupitia mwili.” Lakini “kwa kumtuma Mwana wake mwenyewe akiwa katika mfano wa mwili wenye dhambi” na kwa kumtoa kuwa dhabihu ya ukombozi, Mungu “aliihukumu dhambi katika mwili,” na hivyo kushinda tatizo la ‘Sheria kutokuwa na uwezo.’ Kwa sababu hiyo, Wakristo watiwa-mafuta wanahesabiwa kuwa waadilifu kwa msingi wa imani yao katika dhabihu ya ukombozi ya Yesu. Wanahimizwa ‘watembee, si kupatana na mwili, bali kupatana na roho.’ (Soma Waroma 8:3, 4.) Kwa kweli, ni lazima waendelee kufanya hivyo kwa uaminifu mpaka mwisho wa maisha yao duniani ili wapewe “taji la uzima.”—Ufu. 2:10.
-
-
Tembea Kupatana na Roho ili Upate Uzima na AmaniMnara wa Mlinzi—2011 | Novemba 15
-
-
10. Tunaongozwa jinsi gani na sheria ya dhambi na kifo?
10 Mtume Paulo aliandika hivi: “Kupitia mtu mmoja dhambi iliingia katika ulimwengu na kifo kupitia dhambi, na hivyo kifo kikaenea kwa watu wote kwa sababu wote walikuwa wamefanya dhambi.” (Rom. 5:12) Tukiwa wazao wa Adamu, sisi sote tunaongozwa na sheria ya dhambi na kifo. Mwili wetu wenye dhambi unatuchochea sikuzote kufanya mambo yasiyompendeza Mungu, lakini mambo hayo yanaongoza tu kwenye kifo. Katika barua yake kwa Wagalatia, Paulo aliyaita matendo na tabia kama hizo kuwa “matendo ya mwili.” Kisha akaongeza hivi: “Wale walio na mazoea ya kufanya mambo ya namna hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu.” (Gal. 5:19-21) Watu wa aina hiyo ni sawa na wale wanaotembea kupatana na mwili. (Rom. 8:4) ‘Mambo yanayowaongoza’ na ‘viwango wanavyofuata maishani’ ni vya kimwili kabisa. Je, ni wale tu ambao wanafanya uasherati, kuabudu sanamu, kuwasiliana na pepo, au kutenda dhambi nyingine nzito ndio wanaotembea kupatana na mwili? Hapana, kwa kuwa matendo ya mwili yanatia ndani pia mambo ambayo huenda wengine wakayaona kuwa tu kasoro za utu, kama vile wivu, milipuko ya hasira, ugomvi, na kuwaonea wengine kijicho. Ni nani anayeweza kusema kwamba yeye ameacha kabisa kutembea kupatana na mwili?
-
-
Tembea Kupatana na Roho ili Upate Uzima na AmaniMnara wa Mlinzi—2011 | Novemba 15
-
-
12 Hali yetu ni kama ya mtu anayetibiwa ugonjwa mbaya. Ikiwa tunataka kupona kabisa ni lazima tufuate maagizo ya daktari. Ingawa kuwa na imani katika dhabihu ya ukombozi kunaweza kutuweka huru kutokana na sheria ya dhambi na kifo, bado sisi si wakamilifu na tuna dhambi. Mengi zaidi yanahusika ili kuwa na afya nzuri ya kiroho na kupata kibali na baraka za Mungu. Kuhusu kutimiza lile “takwa la uadilifu la Sheria,” Paulo anatuambia pia kwamba ni lazima tutembee kupatana na roho.
Unaweza Kutembeaje Kupatana na Roho?
13. Inamaanisha nini kutembea kupatana na roho?
13 Tunapotembea, tunasonga hatua kwa hatua kuelekea mahali fulani ambapo tunakusudia kufika. Hivyo, ili kutembea kupatana na roho tunahitaji kuendelea kufanya maendeleo ya kiroho, lakini hilo halimaanishi tunafikia ukamilifu wa kiroho. (1 Tim. 4:15) Ni lazima tujitahidi kwa kadiri ya uwezo wetu kutembea, au kuishi, kupatana na mwongozo wa roho. “Kutembea kwa roho” kunatuongoza kupata kibali cha Mungu.—Gal. 5:16.
-