Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kila Mtu Atakuwa Huru
    Mnara wa Mlinzi—1999 | Mei 1
    • “Kufunuliwa kwa Wana wa Mungu”

      Yehova alitiisha viumbe chini ya ubatili “juu ya msingi wa tumaini” ili siku moja, familia ya kibinadamu ipate kurudishiwa uhuru kupitia utendaji wa “wana wa Mungu.” Hao “wana wa Mungu” ni nani? Hao ni wanafunzi wa Yesu Kristo ambao, sawa na ‘viumbe vingine vya kibinadamu,’ huzaliwa wakiwa chini ya utumwa wa dhambi na kutokamilika. Kupitia kuzaliwa, wao hawana mahali pafaapo katika familia ya Mungu ya ulimwengu wote, iliyo safi na kamilifu. Lakini Yehova huwafanyia jambo fulani lenye kutokeza. Kupitia dhabihu ya fidia ya Yesu Kristo, Yeye huwaweka huru kutoka katika utumwa wa dhambi iliyorithiwa na huwatangaza kuwa “waadilifu,” au safi kiroho. (1 Wakorintho 6:11) Kisha anawafanya kuwa “wana wa Mungu,” akiwarudisha tena katika familia yake ya ulimwengu wote.—Waroma 8:14-17.

      Wakiwa wamefanywa na Yehova kuwa wana wake, watakuwa na pendeleo tukufu. Watakuwa “makuhani kwa Mungu wetu nao watatawala wakiwa wafalme juu ya dunia,” pamoja na Yesu Kristo wakiwa sehemu ya Ufalme, au serikali ya Mungu ya kimbingu. (Ufunuo 5:9, 10; 14:1-4) Hii ni serikali inayosimamishwa imara juu ya kanuni za uhuru na haki—si juu ya uonevu na udhalimu. (Isaya 9:6, 7; 61:1-4) Mtume Paulo asema kwamba hawa wana wa Mungu ni washiriki wa Yesu, ‘mbegu ya Abrahamu’ iliyoahidiwa muda mrefu uliopita. (Wagalatia 3:16, 26, 29) Wakiwa mbegu ya Abrahamu, wana fungu muhimu katika kutimizwa kwa ahadi ya Mungu aliyomtolea Abrahamu rafiki yake. Sehemu moja ya ahadi hiyo ni kwamba kupitia mbegu ya Abrahamu (au, uzao), “mataifa yote ya dunia watajibarikia.”—Mwanzo 22:18.

  • Kila Mtu Atakuwa Huru
    Mnara wa Mlinzi—1999 | Mei 1
    • “Kufunuliwa kwa wana wa Mungu” kunaanza lini? Hivi karibuni sana, wakati Yehova anapowadhihirishia watu wote ni nani ambao ni wana wa Mungu. Huo utakuwa wakati ambapo “wana” hawa, wenye kufufuliwa kwenye makao ya kiroho, watashirikiana na Yesu Kristo katika kuondolea dunia hii uovu na uonevu kwenye vita ya Mungu ya Har–Magedoni. (Danieli 2:44; 7:13, 14, 27; Ufunuo 2:26, 27; 16:16; 17:14; 19:11-21) Kila mahali twaona uthibitisho wenye kuongezeka kwamba tumeingia ndani sana katika “siku za mwisho,” wakati ule muda mrefu ambao Mungu amevumilia uasi pamoja na matokeo yake maovu utakoma.— 2 Timotheo 3:1-5; Mathayo 24:3-31.

  • Kila Mtu Atakuwa Huru
    Mnara wa Mlinzi—1999 | Mei 1
    • ‘Unapongojea kufunuliwa kwa wana wa Mungu,’ unaweza kusitawisha uhakika ambao mtume Paulo alikuwa nao katika utunzaji wenye ulinzi na utegemezo wa Kristo, hata wakati ambapo mateso na ukosefu wa haki waonekana kuwa usioweza kuvumilika. Baada ya kuzungumzia kufunuliwa kwa wana wa Mungu, Paulo aliuliza: “Nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je, ni dhiki au taabu au mnyanyaso au njaa au uchi au hatari au upanga?” (Waroma 8:35) Bila shaka, kwa kutumia maneno ya Rousseau, Wakristo wa siku ya Paulo walikuwa wangali “watumwa” wa mambo yenye kukandamiza ya aina moja au nyingine. Walikuwa ‘wakiuawa mchana kutwa’ kama “kondoo wa kuchinjwa.” (Waroma 8:36) Je, waliruhusu jambo hilo liwashinde?

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki