-
Kushangilia Katika Tumaini LetuMnara wa Mlinzi—2012 | Machi 15
-
-
10, 11. (a) Kondoo wengine wana tumaini gani? (b) Kutimizwa kwa tumaini linalohusiana na dunia kunahusiana jinsi gani na Kristo na “kufunuliwa kwa wana wa Mungu”?
10 Mtume Paulo aliandika kuhusu tumaini tukufu la “wana wa Mungu” waliozaliwa kwa roho wakiwa “warithi pamoja” na Kristo. Kisha alitaja tumaini zuri ajabu ambalo Yehova anauahidi umati usio na hesabu wa kondoo wengine: “Uumbaji [wanadamu] unangojea na kutazamia kwa hamu kufunuliwa kwa wana wa Mungu [watiwa-mafuta]. Kwa maana uumbaji ulitiishwa chini ya ubatili, si kwa mapenzi yake wenyewe bali kupitia yeye aliyeutiisha hivyo, juu ya msingi wa tumaini kwamba uumbaji wenyewe pia utawekwa huru kutoka katika utumwa wa uharibifu na kuwa na uhuru wenye utukufu wa watoto wa Mungu.”—Rom. 8:14-21.
-
-
Kushangilia Katika Tumaini LetuMnara wa Mlinzi—2012 | Machi 15
-
-
12. Kufunuliwa kwa watiwa-mafuta kutawaletea wanadamu manufaa gani mazuri?
12 “Uumbaji” wa kibinadamu utapata kitulizo kikubwa kama nini wakati wa Utawala wa ile Miaka Elfu Moja wa Kristo! Wakati huo, “wana wa Mungu” waliotukuzwa ‘watafunuliwa’ hata zaidi watakapotenda wakiwa makuhani pamoja na Kristo, wakitumia faida za dhabihu ya fidia ya Yesu kwa ajili ya wanadamu. Wakiwa raia wa Ufalme wa mbinguni, “uumbaji” wa kibinadamu utaanza kushuhudia ukombozi kutokana na matokeo ya dhambi na kifo. Hatua kwa hatua wanadamu watiifu ‘watawekwa huru kutoka katika utumwa wa uharibifu.’ Ikiwa wataendelea kuwa waaminifu kwa Yehova wakati wa ile miaka Elfu Moja na wakati wa jaribu litakalokuja mwishoni mwa miaka hiyo, majina yao yataandikwa kwa njia ya kudumu katika “kitabu cha uzima.” Wataingia katika “uhuru wenye utukufu wa watoto wa Mungu.” (Ufu. 20:7, 8, 11, 12) Kwa kweli, hilo ni tumaini zuri ajabu!
-