Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yubile ya Kikristo Yafikia Upeo Katika Mileani
    Mnara wa Mlinzi—1987 | Januari 1
    • 5 Yaliyo ya maana katika habari hii ni m, neno ya mtume Paulo kwenye Warumi 8:19-21: “Viumbe vyote pia vinatazamia kwa shauku nyingi kufunuliwa kwa wana wa Mungu. Kwa maana viumbe vyote pia vilitiishwa chini ya ubatili [vikiwa vyenye dhambi na visivyoweza kuondolea mbali dhambi kabisa].” Ndipo Paulo alipokazia kwamba kuna “tumaini; kwa kuwa viumbe vyenyewe navyo vitawekwa huru na kutolewa katika utumwa wa uharibifu, hata viingie katika uhuru w utukufu wa watoto wa Mungu.” Basi, uhuru huo si kwa wale tu wanaokuwa “watoto wa Mungu” mbinguni. Maneno yaliyozoeleka kwenye Yohana 3:16 yanathibitisha jambo hilo. Na, kama ilivyotajwa, mtume Yohana mpakwa-mafuta alisema kwamba Kristo alikufa “kwa dhambi zetu; wala si kwa dhambi zetu tu, bali na kwa dhambi za ulimwengu wote.’—1 Yohana 2:2.

  • Yubile ya Kikristo Yafikia Upeo Katika Mileani
    Mnara wa Mlinzi—1987 | Januari 1
    • 19, 20. Shetani na mashetani watajaribuje kukatiza baraka zenye kutokana na Yubile ya Mileani, lakini matokeo yatakuwa nini?

      19 Andiko la Ufunuo 20:1-3 linatabiri kwamba Shetani Ibilisi, mtawala wa vikosi vya mashetani, atakuwa ameondoshwa uwanjani kwa muda wa ile miaka elfu ya utawala wa Kristo juu ya wanadamu. Mwishoni mwa ile Mileani, wakati Ibilisi na mashetani wake watakaporuhusiwa kwa muda mfupi wajitokeze, roho hao waovu wataiona dunia, si ikiwa katika hali walimoiacha ikiwa, bali ikiwa paradiso ya duniani pote yenye uzuri usioelezeka. Wataiona dunia ikiwa imekaliwa na ule “mkutano mkubwa” wenye uaminifu na mabilioni ya wafu wa kibinadamu watakaokuwa wamefufuliwa ambao Yesu Kristo alifia akiwa dhabihu ya ukombozi. Kufikia mwishoni mwa Mileani ile Yubile ya Kikristo itakuwa imetimiza kusudi layo la kufungua wanadamu kwa ukamili katika matokeo ya dhambi. (Warumi 8:21) Lingekuwa tendo la kiibilisi na lenye aibu sana kama nini mtu ye yote akijaribu kuharibu hali hiyo nzuri sana! Lakini kwa ruhusa ya Mungu Mwenye Nguvu Zote, Ibilisi atafanya jaribio la mwisho la kutenda hivyo, naye atapiga kwa dharuba akiwa na uchungu wenye kasirani. Kwa sababu hiyo imeandikwa hivi kwenye Ufunuo 20:7-10, 14.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
    Mnara wa Mlinzi—1987 | Januari 1
    • Ijapokuwa hivyo, zingatia kwamba Yubile ulikuwa hasa mwaka wa watu kufunguliwa na kurudishwa katika hali za kwanza. Kwa sehemu kubwa lile juma la uumbaji linahusiana na Dunia-sayari na usitawi wayo. Lakini kwa habari ya kuendelea kutimia kwa kusudi la Mungu kwa wanadamu duniani, tufe (dunia) lenyewe halikuuzwa ndani ya utumwa na hivyo halimo katika uhitaji wa ukombozi. Jamii ya wanadamu ndiyo inayouhitaji, na wanadamu wamekuwapo, si kwa miaka 49,000 bali kwa karibu miaka 6,000. Biblia inaonyesha kwamba wakati fulani baada ya Adamu na Hawa kuumbwa, wao walimwasi Mungu, hivyo wakaingia ndani ya uteka wa dhambi, kutokamilika, na kifo. Kulingana na Warumi 8:20, 21, Yehova Mungu anakusudia kukomboa jamii ya wanadamu wanaoamini watoke katika utumwa huo. Matokeo ni kwamba, waabudu wa kweli duniani ‘watawekwa huru na kutolewa katika utumwa wa uharibifu, hata waingie katika uhuru wa utukufu wa watoto wa Mungu —Ona pia Warumi 6:23.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki