Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Je, Kuna Kitu Kinachoweza “Kututenga na Upendo wa Mungu”?
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Agosti 1
    • Mkaribie Mungu

      Je, Kuna Kitu Kinachoweza “Kututenga na Upendo wa Mungu”?

      Waroma 8:38, 39

      NI NANI kati yetu ambaye hahitaji kupendwa? Kwa kweli, sisi tunajihisi vizuri tunapopendwa na watu wa familia na marafiki. Hata hivyo, inasikitisha kwamba mahusiano kati ya wanadamu yanaweza kuvunjika kwa urahisi au kubadilika kulingana na hali. Wapendwa wetu wanaweza kutuumiza, kutuacha, au hata kutukataa. Lakini, kuna mtu ambaye ana upendo wa kudumu. Upendo ambao Yehova Mungu anawaonyesha waabudu wake unaelezewa vizuri katika Waroma 8:38, 39.

  • Je, Kuna Kitu Kinachoweza “Kututenga na Upendo wa Mungu”?
    Mnara wa Mlinzi—2008 | Agosti 1
    • “Wala kimo wala kina.” Yehova anawapenda watu wake ingawa wana viwango mbalimbali vya maisha, iwe wanaishi maisha ya hali ya juu au ya chini.

      “Wala uumbaji mwingine wowote.” Kwa maneno hayo yanayotia ndani kila kitu, Paulo anasema kwamba hakuna kitu chochote kinachoweza kuwatenga waabudu washikamanifu na upendo wa Yehova.

      Tofauti na upendo wa mwanadamu ambao unaweza kubadilika au kufifia, upendo wa Mungu kuelekea wale wanaomwamini kabisa hauwezi kubadilika; upendo huo ni wa milele. Bila shaka, kujua hilo kunatuchochea kumkaribia Yehova na kutufanya tujitahidi kabisa kuthibitisha kwamba tunampenda.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki