-
Ni Nani Atakayetutenganisha na Upendo wa Mungu?Mnara wa Mlinzi—2001 | Oktoba 15
-
-
14. Kwa nini Paulo alikuwa na hakika kwamba Mungu anawapenda Wakristo licha ya magumu ambayo huenda yakawapata?
14 Soma Waroma 8:38, 39. Ni nini kilichomhakikishia Paulo kwamba hakuna chochote kiwezacho kutenganisha Wakristo na upendo wa Mungu? Yaelekea mambo yaliyompata Paulo akiwa kwenye huduma yaliimarisha uhakika wake kwamba magumu hayawezi kuathiri upendo wa Mungu kwetu. (2 Wakorintho 11:23-27; Wafilipi 4:13) Pia, Paulo alijua kusudi la milele la Yehova na jinsi alivyoshughulika na watu Wake zamani. Je, kifo kinaweza kushinda upendo wa Mungu kwa wale ambao wamemtumikia kwa uaminifu-mshikamanifu? La, hasha! Waaminifu hao wanaokufa wataendelea kuishi katika kumbukumbu kamilifu ya Mungu, naye atawafufua katika wakati ufaao.—Luka 20:37, 38; 1 Wakorintho 15:22-26.
-
-
Ni Nani Atakayetutenganisha na Upendo wa Mungu?Mnara wa Mlinzi—2001 | Oktoba 15
-
-
16 Tukiwa Wakristo, hatuna haja ya kuogopa kwamba yoyote kati ya yale ambayo Paulo aliyaita “mambo yaliyo hapa sasa,” yaani, matukio na hali za mfumo huu wa mambo wala “mambo yatakayokuja” baadaye, yanaweza kuvunja upendo wa Mungu kwa watu wake. Japo wenye mamlaka mbinguni na duniani hupigana nasi, upendo mwaminifu-mshikamanifu wa Mungu unatutegemeza. Paulo alikazia kwamba upendo wa Mungu hauwezi kuzuiwa na “kimo wala kina.” Naam, hakuna kitu chochote kinachoonekana kuwa chenye kuvunja moyo au chenye nguvu kutushinda, ambacho kinaweza kututenganisha na upendo wa Mungu; wala hakuna uumbaji mwingine wowote uwezao kuharibu uhusiano wa Muumba pamoja na watumishi wake waaminifu. Upendo wa Mungu haushindwi kamwe; ni wa milele.—1 Wakorintho 13:8.
-