-
Ujuzi wa Kimbele, Agizo la KimbeleUfahamu wa Kina wa Maandiko
-
-
Maoni ya ile imani ya kuwa imeandikwa kimbele. Maoni ya kwamba matumizi ya Mungu ya ujuzi wa kimbele hayana kipimo na kwamba yeye huagiza kimbele mwendo na hatima ya kila mtu mmoja-mmoja ndiyo ile imani ya kuwa imeandikwa kimbele. Wanaoitetea husema kwamba kwa vile yeye ni Mungu na ni mkamilifu mambo hayo yanamtaka awe mjua-yote, si kwa habari ya wakati uliopita na wakati uliopo bali pia kuhusiana na wakati ujao. Kulingana na dhana hiyo, akikosa kujua kimbele mambo yote kutia na lililo dogo zaidi jambo hilo lingekuwa ni uthibitisho wa kutokamilika. Mifano kama vile kisa cha wana-mapacha wa Isaka, Esau na Yakobo, hutumiwa kuwa uthibitisho wa kwamba Mungu huagiza kimbele juu ya viumbe kabla havijazaliwa. (Ro 9:10-13); na maandiko kama vile Waefeso 1:4, 5 hutajwa kuwa uthibitisho wa kwamba Mungu alijua kimbele na kuagiza kimbele ni nini utakaokuwa wakati ujao wa viumbe vyake vyote hata kabla ya mwanzo wa uumbaji.
-
-
Ujuzi wa Kimbele, Agizo la KimbeleUfahamu wa Kina wa Maandiko
-
-
Katika visa vya Samsoni, Yeremia, na Yohana Mbatizaji, Yehova alitumia ujuzi wa kimbele kabla hawajazaliwa. Hata hivyo, ujuzi huo wa kimbele haukutaja hatima yao mwishowe ingekuwa nini. Badala yake, kwa msingi wa ujuzi huo wa kimbele, Yehova aliagiza kimbele kwamba Samsoni anapaswa kuishi kulingana na nadhiri ya Wanadhiri na alipaswa kuanzisha ukombozi wa Israeli kutoka kwa Wafilisti, kwamba Yeremia alipaswa kutumikia akiwa nabii, na kwamba Yohana Mbatizaji alipaswa kufanya kazi ya matayarisho akiwa mtangulizi wa Masihi. (Amu 13:3-5; Yer 1:5; Lu 1:13-17) Ingawa walikuwa wamependelewa sana kwa kuwa na mapendeleo hayo, hilo halikuwapa uhakikisho kwamba wangepata wokovu wa milele au hata kwamba wangebaki waaminifu hadi kifo (japo wote watatu walifanya hivyo). Kwa hiyo, Yehova alitabiri kwamba mmoja kati ya wana wengi wa Daudi angeitwa Sulemani naye aliagiza kimbele kwamba Sulemani angetumiwa kujenga hekalu. (2Sa 7:12, 13; 1Fa 6:12; 1Nya 22:6-19) Hata hivyo, japo alipendelewa katika njia hiyo na hata kupendelewa kuandika vitabu fulani vya Maandiko Matakatifu, bado Sulemani aliangukia uasi-imani katika miaka yake ya baadaye.—1Fa 11:4, 9-11.
-