-
Mungu Ni Nani?Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
4. Yehova anataka ujue na kulitumia jina lake
Ni nini kinachoonyesha kwamba Yehova anataka ulijue jina lake? Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali haya:
Unafikiri Yehova anataka watu walijue jina lake? Kwa nini?
Yehova anataka watu walitumie jina lake. Soma Waroma 10:13, kisha mzungumzie maswali haya:
Kwa nini tunapaswa kutumia jina Yehova?
Wewe unahisije mtu anapokumbuka jina lako na kulitumia?
Unafikiri Yehova anahisije unapolitumia jina lake?
-
-
Jinsi Dini za Uwongo Zinavyopotosha Ukweli Kumhusu MunguFurahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
-
-
1. Mafundisho ya dini za uwongo yanapotoshaje ukweli kumhusu Mungu?
Dini za uwongo “[zimebadili] kweli ya Mungu kwa ajili ya uwongo.” (Waroma 1:25) Kwa mfano, dini nyingi hazifundishi wafuasi wake jina la Mungu. Hata hivyo, Biblia inasema kwamba lazima watu walitumie jina la Mungu. (Waroma 10:13, 14) Jambo baya linapotokea, baadhi ya viongozi wa dini husema ni mapenzi ya Mungu. Lakini huo ni uwongo. Mungu hasababishi kamwe mambo maovu. (Soma Yakobo 1:13.) Inasikitisha kwamba uwongo wa dini umefanya iwe vigumu kwa watu kumpenda Mungu.
-