-
Mkono wa Yehova Haujawa MfupiUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
17. Mkombozi wa Sayuni ni nani, na anakomboa Sayuni lini?
17 Chini ya Sheria ya Musa, Mwisraeli aliyejiuza utumwani angeweza kununuliwa na mkombozi ili atoke utumwani. Mapema katika kitabu cha unabii cha Isaya, Yehova ameonyeshwa kuwa Mkombozi wa watu mmoja-mmoja wanaotubu. (Isaya 48:17) Sasa anaelezwa tena kuwa Mkombozi wa watu wanaotubu. Isaya anaandika hivi kuhusu ahadi ya Yehova: “Mkombozi atakuja Sayuni, kwao waachao maasi yao katika Yakobo, asema BWANA.” (Isaya 59:20) Ahadi hiyo yenye kutuliza moyo inatimizwa mwaka wa 537 K.W.K. Lakini ina utimizo zaidi. Mtume Paulo alinukuu maneno hayo katika fasiri ya Septuagint, akayatumia kuwahusu Wakristo. Aliandika hivi: “Kwa namna hii Israeli wote wataokolewa. Kama vile imeandikwa: ‘Mkombozi atakuja kutoka Zayoni na kugeuzia mbali mazoea ya kutomwogopa Mungu yatoke kwa Yakobo. Na hili ndilo agano kwa upande wangu pamoja nao, niondoleapo mbali dhambi zao.” (Waroma 11:26, 27) Kwa kweli, unabii wa Isaya unatumika hadi wakati wetu na hata baada ya hapo. Jinsi gani?
-
-
Mkono wa Yehova Haujawa MfupiUnabii wa Isaya II—Nuru kwa Wanadamu Wote
-
-
19. Yehova anafanya agano gani pamoja na Israeli wa Mungu?
19 Sasa Yehova anafanya agano pamoja na Israeli wa Mungu. Tunasoma hivi: “Tena katika habari zangu, hili ndilo agano langu nao, asema BWANA; roho yangu iliyo juu yako, na maneno yangu niliyoyatia kinywani mwako, hayataondoka kinywani mwako, wala kinywani mwa wana [“wazao,” “NW”] wako, wala kinywani mwa wajukuu wako, asema BWANA, tangu leo na hata milele.” (Isaya 59:21) Iwe maneno hayo yalitumika au hayakutumika kumhusu Isaya mwenyewe, hakika yalitimizwa katika Yesu, aliyehakikishiwa kwamba “ataona uzao wake.” (Isaya 53:10) Yesu alisema yale aliyokuwa amejifunza kutoka kwa Yehova, na roho ya Yehova ilikaa juu yake. (Yohana 1:18; 7:16) Basi ni vizuri kwamba hata ndugu zake na warithi wenzake, ambao ni washirika wa Israeli wa Mungu, wanapokea roho takatifu ya Yehova na kuhubiri ujumbe ambao wamejifunza kutoka kwa Baba yao wa kimbingu. Wote ‘wamefundishwa na Yehova.’ (Isaya 54:13; Luka 12:12; Matendo 2:38) Iwe ni kupitia Isaya au ni kupitia Yesu ambaye Isaya anamfananisha kiunabii, sasa Yehova anafanya agano kwamba hatabadilisha kamwe nafasi yao ichukuliwe na watu wengine, bali atawatumia milele wakiwa mashahidi wake. (Isaya 43:10) Hata hivyo, “wazao” wao ambao pia wanafaidika na agano hilo ni akina nani?
-