-
3 | Ondoa Chuki Akilini MwakoMnara wa Mlinzi (Toleo la Watu wote)—2022 | Na. 1
-
-
Biblia Inasema:
“Mgeuzwe kwa kufanya upya akili yenu, ili mjihakikishie wenyewe mapenzi ya Mungu yaliyo mema na yenye kukubalika na makamilifu.”—WAROMA 12:2.
Inamaanisha Nini?
Mambo tunayowaza ni muhimu kwa Mungu. (Yeremia 17:10) Tunahitaji kufanya mengi zaidi ya kuepuka kusema au kufanya jambo linaloonyesha kwamba tuna chuki. Chuki huanzia akilini na moyoni. Hivyo, tunapaswa kuondoa dalili yoyote ya chuki akilini na moyoni. Tukifanya hivyo tutakuwa ‘tumegeuzwa’ kikweli na kushinda chuki.
-